Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Richard Phillip Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. RICHARD P. MBOGO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa nafasi. Kwanza nianze kumpongeza Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri wake na watendaji wote katika Wizara ya Fedha na Mipango, kwa kazi ambazo wameendelea kuifanya. Jambo la kwanza ambalo niende nalo kwanza nimpongeze Mheshimiwa Rais, Dkt. Pombe John Magufuli kwa hotuba yake ya jana ambapo amegusia Benki ya Wakulima jinsi gani inavyofanya kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mwaka huu tukijadili bajeti ya Wizara ya Kilimo na hata mwaka 2017 nilitoa angalizo kwamba miaka ya 1980 tuliwahi kuanzisha Benki ya Wakulima ambayo sasa hivi ndiyo inaitwa CRDB lakini matokeo yake ikahama kwenye lengo na imekuwa benki ya biashara.

Sasa angalizo hilo jana Mheshimiwa Rais amelielezea vizuri kabisa na hii benki iliyoko sasa hivi tuliyoifufua TIDB iende kule mikoani na kila Mkoa na fedha ziende. Kwa hiyo, nampongeza sana Mheshimiwa Rais kwa kuliona hili na kulisimamia kwa ukaribu kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba niguse kidogo jambo moja la 1.5 trillion ambalo linazungumziwa na wenzetu. Kimsingi kama umekusanya shilingi 200 ukatumia shilingi 190 unabaki na shilingi 10. Kwa hiyo, ni kuuliza hiyo shilingi 10 imekaa wapi? Kimsingi CAG katika ripoti yake hakusema hii 1.5 trillion haipo, sio hoja. Alieleza tu mapato na matumizi.(Makofi)

Mheshimiwa Spika, katika hii fedha kuna nyingine inatokana na kitu kinaitwa IPSA Accruals. Kwa wale wahasibu wanajua. Kuna Accounting Principles; kuna going concern, kuna monitory unit, historical cost, matching concept, accounting period consistency.

Mheshimiwa Spika, sasa ili kuweza ku-meet ile accounting principles kwa mfano ya matching kwamba umeuza Juni, uripoti Juni; umeuza Machi, uripoti Machi; ndiyo maana zimewekwa hizi accruals kwamba haya ni mapato tarajiwa katika mwaka wa fedha huu, kwa hiyo, unai-record ingawa fedha yake taslimu itaingia mwaka unaofuata. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, na mimi nazungumza nimeifanyia kazi, mimi ni mhasibu. Nime-practice pale Swissport Tanzania, mizigo ambayo imekuja na haijatoka, tulikuwa tunafanya accruals kutokana na kanuni za TRA kwamba mizigo baada ya siku 21 inaenda kupigwa mnada. Kwa hiyo, mnachukua ya miezi miwili mnafanya accruals, mna-record katika mapato, yanaingia kwenye mwaka wa fedha husika halafu amortize mwaka unaofuata. Kwa hiyo, mkitaka shule ya accruals nje.

Mheshimiwa Spika, naomba niende kwenye Ofisi ya Msajili wa Hazina. Ofisi ya Msajili wa Hazina ni muhimu sana. Tuna mashirika na makampuni takribani 270 yanayosimamiwa na hii ofisi. Kimsingi nimeona katika utekelezaji wa bajeti wamepewa fedha ndogo sana asilima 17 tu katika mafungu ambayo tunaenda kupitisha. Sasa uwekezaji uliofanywa na Serikali ni karibuni shilingi trilioni 47, kwa mali zote ambazo Serikali imewekeza katika haya mashirika.

Kwa hiyo, naomba utendaji wa TR uangaliwe kwa kupewa fedha na kuwezeshwa ili waende wakasimamie vizuri. Wakisimamia, maana yake uwekezaji ambao umefanywa na Serikali tutaiona ile return on investment. Kama kuna mashirika yanafanya kwa hasara watasimamia. Naomba pia wapewe fedha ili wawekeze katika mfumo wa kisasa wa TEHAMA, wasitoke physically, watengeneze mfumo wa kuripoti kila mwezi wanaona, ripoti zinaingizwa tu world based, kama mtu yupo Arusha, Bukoba au Mbeya, anaingia kwenye internet anaweka ripoti. Mtu wa Hazina aliyepo Dar es Salaam au Dodoma hapa ana-view na assess na ameweka criteria zake pale anaangalia kwamba performance imekaaje na anachukua hatua haraka.

Mheshimiwa Spika, kingine kwa upande wa ile asilimia 15 ya gross iangaliwe. Kuna mashirika mengine ambayo siyo ya kibiashara, kwa hiyo, yanakusanya na bajeti yao ya uendeshaji ni ndogo. Kwa hiyo, sheria iboreshwe zaidi ili mapato yao yaje yaingie kwenye Serikali na yasaidie katika miradi yetu mbalimbali ya maendeleo.

Mheshimiwa Spika, jambo lingine kuna Kampuni ya UTT PID inayohusiana na miradi ya maendeleo ya miundombinu, nimeona kwenye kitabu na hotuba ya Waziri kwamba wanapima maeneo mbalimbali kama Dodoma sijui Bukoba mtakaba na TPA.

Mheshimiwa Spika, naomba nimwambie Mheshimiwa Waziri kwamba hawa ITT PID they are dying. Mwaka 2017/ 2018 a half year performance wana loss ya 131 million. Kwa hiyo, inaenda kula reserves za nyuma. Wana receivable za almost eight billion. Kwenye five billion wapo watu mbalimbali. Are they collectable? Kwa hiyo, angalia hii. Aidha ufanye compulsory wind-up au voluntary wind-up, usiendelee kupata hasara na mtaji ambao umeshaingia kwa Serikali utaenda utaliwa wote. Hii receivable mkifanya provision, imekula reserve yote ya nyuma.

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na wastaafu, jana liliulizwa swali na Mheshimiwa Lucy na akasema kwamba ni kweli kuna watu wanalipwa shilingi 50,000. Naomba nithibitishe, ni kweli kuna watu wanalipwa shilingi 50,000, mmojawapo ni Augustino Mbalamwezi mwenye Pf. No. 613667 Check No. 27850. Huyu alikuwa Mtumishi wa Posta tangu East Africa analipwa shilingi 50,000, yeye halipwi shilingi 100,000. Kwa hiyo, naomba Wizara na wanasikia, wamlipe arreas zake zote. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuna suala la Dar es Salaam Stock Exchange (DSE), hivi sheria inasemaje kama Bunge limepitisha sheria kwamba Makampuni ya Simu na taasisi nyingine zisajiliwe DSE na mpaka leo hazijasajiliwa, sheria inasemaje? Tumeona kwamba Makampuni ya Simu yanatakiwa yasajiliwe. Vodacom ndiyo ameshaingia, hao wengine mpaka leo kwa nini hawajaingia DSE? Sasa DSE hana meno au ndiyo Wizara kwamba haina meno? Kwa hiyo, tutaomba uje utueleze kwa nini imetokea hivyo?

Mheshimiwa Spika, kuna suala la fedha za ruzuku. Mwezi wa Pili mwaka huu TAMISEMI waliita Wakurugenzi, Maafisa Mipango na Wenyeviti wa Halmashauri waka-review bajeti kwamba waelekeze miradi ya kimkakati ambayo itafanyika na itakamilika na kwamba fedha za ruzuku zitakuja. Mpaka tunavyozungumza hivi, fedha za ruzuku hazijaenda. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa naomba Mheshimiwa Waziri atuambie, kwa nini hajatekeleza angalau kwa asilimia 50? Tumeaminisha wananchi kwamba tutajenga kituo cha afya, tutajenga sekondari, tutaboresha matundu ya vyoo kwa fedha hizi za ruzuku, lakini mpaka leo hii hata asilimia 50 hazijaenda na mwaka wa fedha ndiyo huu unaishia. Tutaomba utupe hayo majibu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuna suala la kurasimisha sekta zisizo rasmi. Katika hotuba ya bajeti ya mwaka 2017 wakati wa bajeti yako ya mwaka 2017/2018 ulieleza vizuri kabisa kwamba watasajiliwa, watapewa vitambulisho na TRA itaenda kukusanya kodi. Sasa huu mchakato wa kutoa vitambulisho na kutambulika hii sekta isiyo rasmi, ndogo ndogo lakini ni nyingi, utapata mapato huko na utaongeza. Utekelezaji wake mpaka leo umefikia wapi? Tunaona Kariakoo imejaa Machinga, utaratibu mzuri hauonekani, barabara zimefungwa kwa biashara, hata hapo Dodoma pale Nyerere Square kila jioni watu wanafanya biashara. Sasa hawa, ni ndogo ndogo wakitoa, lakini utaingiza mapato. Hebu Mheshimiwa Waziri atuambie imefikia wapi? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuna suala la hii Bodi ya Michezo ya Kubahatisha, wengi wamezungumza na ninaomba tu kwamba hebu tuone kutoka kwenye…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.