Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Halima James Mdee

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya ripoti ya CAG kutoka Machi, 2018, Naibu Spika alirekodiwa akisema hapa Bungeni kwamba kuzungumzia taarifa ya CAG ni suala halali na kila mtu ana haki ya kuzungumzia ripoti ya CAG. (Makofi)

Kwa mantiki hiyo, ruling ya Spika ni kwamba Wabunge tuna haki ya kujiachia kwenye ripoti ya CAG na kwa mantiki hiyo tunamtaka Waziri wa Fedha akijibu hoja zake atuambie shilingi trilioni 1.5 iko wapi. Tunamtaka Waziri wa Fedha akijibu hoja zake atuambie shilingi bilioni 200 mliyopeleka Zanzibar iko wapi, ilipelekwa lini, kwa usafiri gani na ilifanya nini? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa anapoteza muda hana mpya bwana, anarudia kulekule anapoteza muda…

KUHUSU UTARATIBU . . .

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Mwenyekiti, namwambia hivi Mheshimiwa Dkt. Magufuli ameshakusikia unavyopambana tulia kashasikia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, huu mtindo wa makusanyo kutolewa yakiwa pungufu, ukirejea hata ripoti ya CAG ya mwaka iliyotolewa Machi, 2017 ukurasa wa 42 unatuambia walikusanya Serikali shilingi bilioni 21.1 wakatumia shilingi bilioni 20; kwa hiyo, hii inatupa tafsiri gani kwamba ni utamaduni wa Serikali hii ya CCM wanakusanya mapato, wanafanya matumizi halafu kuna kachenji kanabaki wanajua wanakafanyia nini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunasisitiza Waziri wa Fedha ndio unadhamana za fedha za nchi hii 2015/2016 ripoti iliyotolewa Machi, 2017 kuna katrilioni moja kalikuwa hakaelewiki kako wapi, mwaka 2017/2018 ripoti imetolea Machi 18 shilingi trilioni 1.5 mtatujibu leo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili tunataka Waziri wa Fedha akija atuambie zile fedha za makinikia ziko wapi? Mnakumbuka mwaka 2017 Rais aliunda Tume mbili nchi ikasimama tv zote live, tukawaambia Watanzania kwamba ACACIA Mining hawajalipa kodi wamejificha kwa kuibia Serikali kuanzia mwaka 2000 mpaka mwaka 2017.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mkaliambia Taifa tuna idai ACACIA shilingi trilioni 424 kodi. Leo mpaka sisi tukawaambia jamani hapa shida siyo ACACIA, shida ni Serikali ya CCM na mikataba mibovu ambayo inaimaliza nchi. Mwaka mmoja baadae mbele ya Bunge hili Tukufu anasimama Mheshimiwa Profesa Kabudi mwalimu wangu na mpaka naona aibu kuwa na mwalimu kama yeye, anasema, anatuambia eti hatuwezi kutoa siri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ya Mheshimiwa Magufuli ilisema unaidai ACACIA Mheshimiwa Mwenyekiti, shilingi trilioni 400 leo Waziri wa Sheria anatuambia eti anaona aibu wakisema wanaotudai watakuja kutudai. Hivi wakati mnatangaza hiyo shilingi trilioni 400 waliokuwa wanatudai hawakujua, sasa ni hivi Serikali muwaambie watanzania kwamba mliwadanganya.