Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Uchambuzi wa Sheria Ndogo zilizowasilishwa katika Mkutano wa Kumi na Kumi na Moja wa Bunge

Hon. Andrew John Chenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Uchambuzi wa Sheria Ndogo zilizowasilishwa katika Mkutano wa Kumi na Kumi na Moja wa Bunge

MHE. ANDREW J. CHENGE – MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA SHERIA NDOGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru sana kwa kunipatia nafasi niweze kuhitimisha hoja yangu iliyo mbele ya Bunge lako. Nitajitahidi niongee kwa kifupi sana kwa sababu ya muda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niwashukuru sana Waheshimiwa Wabunge wote kumi waliopata nafasi ya kuchangia kwa kuongea humu Bungeni na Waheshimiwa Wabunge wawili waliochangia kwa maandishi, niwashukuru sana. Mmeielewa hoja na mmeeleza vizuri changamoto ambazo zipo katika shughuli za sheria ndogo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze na moja la jumla, Waheshimiwa Wabunge ndiyo maana Serikali inapoleta miswada tujitahidi sana tunapoiunga mkono Serikali, maana shughuli za Serikali lazima ziende, lakini tuwe makini sana wanapowaambia kwamba masuala haya tutakwenda kuyaweka kwenye regulations.(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli muswada hauwezi ukafafanua kila aspect lakini ile misingi na mipaka ya utekelezaji wake unataka uione, iwe katika sheria mama na mkifanya hivyo usimamizi wenu kama Bunge, oversight, control, supervision ya sheria ndogo utakuwa na maana sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeona zipo kanuni, sheria ndogo ukiziona unajiuliza hivi…, lakini kwa sababu ni sheria za nchi zinatumika, lakini tukianza vizuri kuwa makini na kile ambacho tunakikasimu then tutakuwa on a good footage. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, limesemewa vizuri sana, kwa nini hizi sheria ndogo zisianze kutumika mpaka hapo utaratibu fulani unapofanyika? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme tu hivi, katika nchi za Madola, tuna mifumo ya aina mbili ya kusimamia madaraka ambayo Bunge limekasimu kwa vyombo vingine. Mfumo wa kwanza unaitwa affirmative resolution procedure yaani unaleta hizo rasimu zako za sheria ndogo unaziweka mezani kabla hazijaanza kutumika na Wabunge ndiyo wanapata nafasi ya kuona kinacholetwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hatua hiyo wanaweza wakasema no, kanuni hizi na hizi au kanuni hii hapana, kwa hiyo, wanakwenda kuirekebisha huko halafu ndiyo inakwenda kuchapishwa kwenye Gazeti la Serikali ianze kutumika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna utaratibu wa pili ambao unaitwa negative resolution procedure ambao sisi Tanzania ndiyo tunaangukia humo, kwamba ukiisoma Sheria yetu ya Tafsiri ya Sheria, na ndiyo maana taarifa ya Kamati inasema udhibiti wa Bunge siyo wa moja kwa moja, unasubiri kwanza ichapishwe kwenye Gazeti la Serikali ili iwe sheria ndogo halafu iwasilishwe Bungeni. Lakini ikishachapishwa imeshaanza kutumika, ndiyo tofauti ile ya affirmative na hii ya negative. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa mmelisema vizuri Waheshimiwa Wabunge Mheshimiwa Rashid Abdallah, Mheshimiwa Hawa Ghasia, Mheshimiwa Zainab na wengine Mheshimiwa Kingu na Mheshimiwa Aida, kila mmoja karibu amegusia Mheshimiwa Ridhiwani wameyagusia, mimi nasema yote haya jamani yanazungumzika, hizi ni sheria zilitungwa na Bunge hili. Tukiona kwamba utaratibu wa negative resolution procedure haujakaa vizuri tunajenga hoja, tunashauriana na Serikali tukielewana tunafanya marekebisho, tu-adopt the negative ni nanii affirmative relation procedure. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa naelewa Mheshimiwa Mdee amelisema vizuri sana Bunge letu halikai kila siku. Lakini unaweza kwa sababu tunajua lini mikutano yetu ya Bunge inapaswa kufanyika. Mnaweza mkajipanga na sheria ikasema wazi except kwa aina fulani ya sheria ndogo za dharura zile maana dharura ni dharura hauwezi ukasema isubiri sijui nini. Unaweka utaratibu ambao unawezesha Bunge kupitia Kamati husika kuweza kuyaangalia haya, mimi nadhani tutakapokuja kuelewana kwa hivyo tutaenda vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niwashukuru sana mlioiona maana hizi ni sheria wala usiseme Sheria Ndogo kwa sababu ni subsidiary, lakini zitatumika na wanachi na zingine is very hash ikikosewa tu kidogo unamuumiza mtu; na hapa nichukue nafasi kumshukuru sana Mheshimiwa kwa kuona busara aliyoiona kwamba turejeshe utaratibu huu na Taarifa za Kamati ziwe zinawasilishwa mara mbili kwa mwaka maana ni sheria zinatumika, tusiruhusu wananchi wanaendelea na vyombo vingine wanaendelea kuumia kwa sababu tu sheria hazijapitiwa na Bunge kupitia Kamati husika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Waheshimiwa Wabunge kundi la sheria ndogo limetajwa kwenye Sheria ya Tafsiri subsidiary legislation means any order, proclamation, rule of court, regulation, notice, by law or instrument made, narudia made under any act or other lawful authority. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, huo ndiyo msingi ni vema tunapoyaangalia haya tuzingatie, sheria ndogo haiwezi ikavika ukuu ambayo haina katika sheria mama. Hiyo misngi ya kutunga sheria na tafsiri haiwezi ikajibika ukuu ambao haina katika sheria mama. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kwa vile Serikali ipo najua nilivyosema kwenye taarifa tunafanya kazi karibu sana na Ofisi ya Waziri Mkuu kupitia Mheshimiwa Jenista Mhagama kama coordinator wa shughuli za Serikali na Chief Whip wa Serikali Bungeni katika shughuli hizi na hili la BASATA niseme namshukuru sana Mheshimiwa Waziri Dkt. Mwakyembe kwa sababu alipofika kwenye Kamati aliliona na akasema kiungwana tu jamani nipeni muda na mtu muungwana akimwambia hivyo lazima na wewe uoneshe uungwana, ndio maana tukasema sisi tutasema tu kwamba ilipaswa ije lakini kwa sababu haijakaa vizuri tumekubaliana itakuja katika Mkutano mwingine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho kwa sababu lazima sasa baadae Bunge litaamua nisome sasa maazimio haya ili Bunge litakapohojiwa lijue linaamua nini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja ya kwanza inahusu dosari ya uandishi wa majedwali ikilinganishwa na vifungu vya sheria.

KWA KUWA katika uchambuzi wa Kamati imebainika kuwa baadhi ya sheria ndogo zinadosari mbalimbali katika majedwari kuhusu vifungu vinavyoanzisha majedwali husika.

NA KWA KUWA kwa mujibu wa kifungu cha 25(2) cha Sheria ya Tafsiri ya Sheria kinabainisha kwamba majedwali ni sehemu ya sheria;

KWA HIYO BASI Bunge linaazimia kwamba Wizara ambazo sheria ndogo zake zimebainika kuwa na dosari katika majedwali zifanyanyiwe marekebisho ili kuondoa dosari hizo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, azimio la pili linahusu kukinzana na masharti ya sheria mama au sheria nyingine za nchi.

KWA KUWA baadhi ya sheria ndogo zilizofanyiwa uchambuzi na Kamati zimebainika kuwa na vifungu vinavyokinzana na masharti ya sheria mama au sheria nyingine za nchi.

NA KWA KUWA kukinzana huko ni kwenda kinyume na masharti ya kifungu cha 36 cha Sheria ya Tafsiri ya Sheria kinachotoa sharti kuwa sheria ndogo kutokwenda kinyume na masharti ya sheria mama.

NA KWA KUWA kukinzana huko kuna ifanya kanuni husika kuwa ni batili kwa kiwango kilichokinzana.

KWA HIYO BASI Bunge linaazimia kwamba Wizara zinazohusika kufanya marekebisho katika sheria ndogo hizo ili kuondoa vifungu vinavyokwenda kinyume na masharti ya sheria mama au sheria nyingine za nchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kutoa hoja.