Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Mwanne Ismail Mchemba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. MWANNE I. MCHEMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, pongezi kwa Waziri, Mheshimiwa Mwigulu Lameck Nchemba; Mheshimiwa Naibu Waziri, William Tate Ole-Nasha; Dkt. Florence Martin Turuka, Katibu Mkuu na Makatibu Wakuu wote wa Wizara hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, ushauri ni kwamba, migogoro ya ardhi, wafugaji, wakulima ni vema Serikali sasa kuchambua sera mbalimbali zinazohusiana na matumizi makubwa kuchunguza mikakati ya utekelezaji wa sera hiyo. Mikakati yote ya Serikali ya kusuluhisha migogoro ya wakulima na wafugaji. Wananchi washirikishwe kutoa mapendekezo yatakayoondoa migogoro iliyopo ili kudumisha mahusiano mazuri kati yao.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wenyeviti wa Vitongoji na Vijiji wapewe elimu ya mahusiano, kutenga maeneo ya wafugaji na wakulima. Elimu kwa wafugaji kufuga kisasa kwa kupunguza mifugo. Majosho ni machache, Serikali ipange katika bajeti hii ongezeko la mabwawa na majosho, ni kero kwa wafugaji.
Mheshimiwa Naibu Spika, matatizo na changamoto. Chuo cha Kilimo Tumbi hakijafanyiwa ukarabati wa miundombinu kwa muda mrefu. Wakufunzi katika Chuo cha Tumbi wachache, madai ya wafanyakazi yalipwe.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu tumbaku; tozo kwenye zao hili la tumbaku ni nyingi, Serikali ifuatilie ili kuwapunguzia wakulima mzigo. Soko la tumbaku ni kero, pamoja na pembejeo kufika kwa wakati.
Mheshimiwa Naibu Spika, machinjio ya Tabora Manispaa yapo katika hali mbaya na hayafai kabisa kwa afya ya wanadamu, pia kuboreshwa kwa bwawa la Igombe ili kuweka mbegu ya samaki ya aina zote. Kutoa elimu ya kufuga samaki kwa wajasiriamali ambao wana vikundi vya ufugaji katika mikoa yetu hapa nchini. Kusambaza mbegu ya alizeti kwa wakulima wote kwenye wakulima wa zao hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, vitendea kazi. Maafisa Ugani wapewe angalau pikipiki hata baiskeli, wapewe motisha ya kazi katika mazingira magumu. Serikali ijenge nyumba za Maafisa Kilimo na Mifugo Vijijini, wakopeshwe mikopo kwa ajili ya kuandaa mashamba darasa kwenye maeneo husika, hali za maisha yao ni mbaya.
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.