Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Uchambuzi wa Sheria Ndogo zilizowasilishwa katika Mkutano wa Kumi na Kumi na Moja wa Bunge

Hon. Elibariki Emmanuel Kingu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Uchambuzi wa Sheria Ndogo zilizowasilishwa katika Mkutano wa Kumi na Kumi na Moja wa Bunge

MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuchangia. Kwanza kabisa ni wazi inajulikana kabisa ya kwamba jukumu la kutunga sheria ni jukumu la Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mujibu wa Katiba. Kinachofanyika kitendo cha ku-delegate mamlaka ya utunzi wa sheria kwenda kwenye mhimili wa executive ni kutokana na ukweli kwamba Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania haliwezi kukaa kila siku na kutunga hizi regulations ambazo zinatumika kwenye mamlaka za Serikali na Serikali Kuu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kimsingi tukiri ya kwamba mimi nikiwa kama moja ya wajumbe wa Kamati ya Sheria Ndogo tumeshuhudia kwa kiwango kikubwa ukosefu wa umakini mkubwa sana sana sana kwa upande wa executive katika utunzi wa sheria na hasa regulation ambazo kimsingi ndizo zinagusa maisha ya wananchi ya kila siku.

Mheshimiwa Mwenyekiti, umakini huu umesababisha sisi kutilia mashaka ni kwa kiwango cha namna gani wananchi wetu wanaweza wakawa vulnerable kuathirika kutokana na matumizi ya regulation ambazo tunaweza tukazipitisha na wakati mwingine kwa kiwango kikubwa zinaletwa hapa zikiwa tayari zimeshakuwa gazetted na ziko kwenye operation.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeshuhudia kanuni nyingi zinatungwa, kanuni inasema hivi lakini ukienda kwenye sheria unakuta ni kitu tofauti hakiendani na kitu hata kimoja kuhusiana na sheria husika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mfano mdogo, ukienda kuangalia GN. 80 ambayo inaongelea habari za Urban Planning Building Regulation ya mwaka 2018; ukienda kusoma kanuni ya tatu inatoa tafsiri ya neno vehicle ambayo kimsingi ukiangalia tafsiri hiyo iko kabisa kinyume na Sheria ya Usalama Barabarani kifungu cha 168.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukizingatia hilo, ukiachilia mbali kanuni hiyo kutoa tafsiri ya neno vehicle tofauti, lakini bado regulation yenyewe inaongelea habari za Urban Planning Building Regulation, sasa mambo ya vehicle kwenye mambo ya urban yanaingiliana wapi? Hii inaonesha kwa kweli kuna ukosefu wa umakini mkubwa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi niiombe Serikali, regulations hizi ndizo zinazotumika ku-govern maisha ya kila siku ya wapiga kura na wananchi wetu. Kama mhimili wa Serikali hautachukulia suala la utungaji wa regulation ni kuwa ni suala serious kama alivyosema dada yangu Mheshimiwa Katimba, kuhakikisha kwamba mnapata manpower na skilled labour ambayo itaweza kusaidia Ofisi ya Mwanasheria na watu wa TAMISEMI katika kuhakikisha kwamba regulation zinazokuja ziweze ku-reflect misingi ya uandishi wa sheria katika nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama hilo halitoshi, bado ukienda katika masuala ya uandishi wa majedwali, katika taratibu za uandishi wa sheria majedwali ni sehemu ya sheria, lakini unaweza ukakuta jambo limezungumzwa ukienda kwenye jedwali halipo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, haya mambo kwa namna moja ama nyingine yasipoangaliwa kwa umakini na kwa trend tuliyonayo ya ku-gazette regulation na kuzifanya zitumike na zinakuja baadae kwa sababu ya wingi italeta madhara makubwa sana kwa wananchi wetu. Nina imani ninayasema haya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ananisikiliza ili kusudi yaweze kufanyiwa kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia pamekuwa na makosa makubwa ambayo yamekuwa yakifanyika. Misingi ya uandishi wa sheria imekuwa ikikiukwa sana, nikiwa na maana ya drafting principles katika uandishi wa regulations. Mfano mdogo unaweza ukaenda kwenye GN. 90, ukienda katika GN. No. 90 utakuta kwenye ile sheria nyuma ya sheria kuna maelezo ambayo ndani ukiangalia hayana explanation yoyote. Ili maelezo yoyote katika sheria yaweze kupata nguvu ya kisheria, lazima yawe na kifungu kinachotoa support ambacho kinayapa maelezo hayo nguvu ya kisheria.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini ukienda katika hiyo sheria niliyoisema katika GN. 90 ambayo kimsingi inaongelea The Urban Planning (Urban Farming) Regulations, 2018 ambayo inayotoka na sheria mama The Urban Planning Act Sura ya 355, ameizungumzia Mheshimiwa Katimba, lakini nyuma ya sheria nenda kasome utakuta kuna maelezo, hakuna kifungu chochote kinachoyapa maelezo hayo nguvu ya kisheria, huu ni udhaifu mkubwa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, nitoe ushauri kwa Serikali. Kwa sababu sisi katika Kamati tume-observe makosa ya kimsingi ambayo kimsingi unaona kabisa ya kwamba kuna ukosefu wa umakini wa hali ya juu katika suala zima la utunzi wa regulation. Niiombe Serikali, kupitia Ofisi ya TAMISEMI, kupitia Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, toeni semina kwa maafisa ili watu wanapofanya kazi zinazoletwa kwenye Bunge tuweze kuona kwamba Mhimili wa Serikali uko serious katika kuandaa regulation ambazo zinatumika kwa wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, niiombe Serikali kwa umakini mkubwa kabisa, ni muda muafaka sasa regulation zetu kabla hazijakuwa gazette, kwa sababu nyingi sisi kama Wabunge ambao tunasimama kwa niaba ya wananchi zinaweza kuleta madhara makubwa kwa wananchi, tuiombe Serikali kabla hawaja- gazetted regulation na kanuni zozote wazilete kwenye Bunge tuweze kuziridhia ndipo ziende zikawe gazetted kwa ajili ya maslahi ya wapiga kura wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, ninaunga mkono hoja nina imani Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali wamesikia na nina imani Ofisi ya TAMISEMI pia wamesikia.