Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Uchambuzi wa Sheria Ndogo zilizowasilishwa katika Mkutano wa Kumi na Kumi na Moja wa Bunge

Hon. Rashid Ali Abdallah

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Tumbe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Uchambuzi wa Sheria Ndogo zilizowasilishwa katika Mkutano wa Kumi na Kumi na Moja wa Bunge

MHE. RASHID ALI ABDALLAH: Mheshimiwa Mwenyekiti, jina langu lilikuwa ni Rashid Ali Abdallah.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kunipa nafasi hii. Pia, nishukuru kwa wasilisho lililotolewa na Mwenyekiti wangu na kufahamika vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Bunge ndicho chombo pekee cha kutunga sheria na mara baada ya kutunga sheria, sheria hii lazima iende ikatekelezwe, na utekelezaji wa sheria hii kunahitajika kuandaliwa kwa kanuni chini ya Ibara ya 97(5) ya Katiba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumesikia jinsi uchambuzi ulivyotolewa na hiyo ndiyo hali halisi ya baadhi tu ya sheria, kanuni ambazo zimeletwa katika Bunge hili. Kwa utaratibu sheria zinatungwa huko zinakotungwa, aidha, Waziri au Wizara yake, lakini zinapitia kwa Mwanasheria Mkuu halafu baaday ndipo zinatangazwa katika Gazeti Rasmi la Serikali na kupewa GN. number. Sheria hizi baada ya hapo zinaendelea kutumika kabla ya kupita kwenye Kamati hii ya Sheria Ndogo. Kwa hiyo, tutaona hapa sheria chache tu ambazo zimewasilishwa kwenye Bunge zina makosa ambayo yamekwenda kinyume na Katiba ya nchi, zimekwenda kinyume na sheria na hata zimekwenda kinyume na haki za binadamu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, utaona trend ilivyo, kwamba sheria ngapi zimepita hapa na sheria ngapi ziko nje zinatumika kimakosa na kwa maana hiyo, tunasema kwamba, sheria hizi nyingi ambazo zinatungwa watungaji hawana uangalifu wa kutosha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu kama ni Halmashauri basi tunao Wanasheria wa Halmashauri, zikitoka kwenye Halmashauri zinakwenda kwa Waziri, zikitoka kwa Waziri zinakwenda kwa Mwanasheria Mkuu, lakini bado makosa yanakuwa makubwa, yanakuwa kinyume na Katiba. Kwa hiyo, tunaona ni jinsi gani kazi inavyofanyika na jinsi gani wananchi wanaumia huko vijijini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme kwamba kama tunabadilisha sheria, Kamati imependekeza sheria ibadilishwe, lakini bado sheria inatumika huko, kwa hiyo huu ni mzunguko. Kwanza uende ukabadilishe sheria, sheria inaendelea kutumika, kwa hiyo haileti maana halisi. Mimi nadhani huu ni mfumo wa Serikali kuweza kutumika sheria kabla ya kupita kwenye Kamati, lakini kuna haja sasa ya mfumo huu kutazama upya kwa sababu, sheria inaumiza wananchi, lakini inatumika na baadaye ndipo sheria inakuja kwenye Bunge na hiyo sio sheria zote ni baadhi tu ya sheria.

Mheshimiwa Mwenyekiti, angalia hizo sheria ambazo ziko huko ni kiasi gani zinakandamiza wananchi hawa? Kuna mazao, ulipaji wa kodi ya mazao, kuna masuala ya uendeshaji wa shughuli mbalimbali za biashara zao, kuna kanuni hizo zinaendelea kutumika, basi wanyonge huko ndio wanaoumia zaidi. Sheria hizi ni za nchi nzima, kila unapokwenda ziko sheria hizi ndogo zinaendelea kutumika na zinaendelea kwa sababu kuna sheria mama inatekelezeka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nina wazo kwamba kwa mujibu wa Katiba Bunge limekasimu madaraka kutunga hizi kanuni, lakini hao ambao wanatunga hawako serious, na makosa haya yataendelea kuwepo.

Mimi nilisema kuna haja ya kubadilisha mfumo huu, sheria zile ambazo ni very serious au ni emergency majesty, ni haraka sana, zinaweza zikaenda, lakini zile sheria ambazo hazina umuhimu sana kabisa, basi ni lazima zipitie kwenye Kamati ya Sheria Ndogo, ili kuhakikisha kwamba, ziko sahihi; lakini tukiendelea na mfumo huu bado Wananchi wataendelea kukandamizwa na hakuna mtu wa kuwasaidia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano hata Serikali nayo inapata matatizo, kuna uendeshaji wa shughuli za petroli. Kama unaendesha shughuli za petroli lazima uwe na kibali, na sheria inasema kama huna kibali basi ni faini isiyopungua shilingi milioni 20. Hata hivyo kanuni inasema kama utaendesha shughuli hizi za petroli bila kibali ni faini ya shilingi milioni tano. Kwa hivyo, hapo tunaona Serikali imepeta hasara kiasi cha shilingi milioni 15 zimeondoka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna kanuni inasema milioni tano; na hiyo, sijui kama imeletwa wakati gani kwenye Bunge. Kwa hiyo, ni kusema kwamba Serikali pia inakosa mapato, lakini pia wananchi nao pia wanakandamizwa na sheria hizi kwa sababu zinakuwa ni kinyume na Katiba na hata pengine wakaenda Mahakamani sheria hizi hazina support yoyote, zinafutwa na kwa maana hiyo ni kupoteza nguvu ya Serikali, kupoteza nguvu ya Wananchi wenyewe walioshitakiwa na haileti tija yoyote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi pendekezo langu ni kwamba, sheria hizi zinagusa Wabunge wote katika majimbo yao na Halmashauri zao. Kuna haja ya kubadili mfumo ili kuhakikisha sheria kwanza zinathitishwa ziko sahihi, lakini pia, ninachokisema mimi na kinachonisikitisha kabisa ni kwamba, kwa nini sheria inapita kwa Mwanasheria Mkuu? Kwa nini sheria inapita kwa Mheshimiwa Waziri?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Waziri anakuja kwenye Kamati basi haelewi ni sheria ipi anakuja kui-defend. Sasa sijui hizi sheria zinakwendaje, hawaeleweki; Waziri unamwambia funua ni sheria gani, anamuuliza Katibu Mkuu, haelewi. Kwa hiyo Mawaziri hawako serious na masuala haya, Mwanasheria Mkuu pia katika ofisi yake hawako serious na katika Halmashauri, Wanasheria wa Halmashauri hawako serious. Kwa hiyo, hii mamlaka waliyopewa hawaietendei haki ni vizuri turudie katika mfumo ambao ni sahihi. Nakushukuru sana.