Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Hon. Othman Omar Haji

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Gando

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

MHE. OTHMAN OMAR HAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, Maendeleo ya Utumishi Wizarani. Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ni Wizara ya Muungano wa pande mbili za Tanganyika na Zanzibar. Wizara imekuwa ikilalamikiwa kwa kutotenda haki kwenye masuala ya utumishi ndani ya Wizara. Watumishi walio wengi ni wa upande mmoja wa Muungano. Wakati Wazanzibari wanapohoji Mawaziri wenye dhamana huwa wanatoa hoja ya kuwa utumishi huhitaji weledi na vigezo. Je, Wazanzibari wamekosa sifa hiyo?

Mheshimiwa Naibu Spika, Kituo cha Mikutano cha Kimataifa (AICC). Wakati AICC inatimiza karibu miaka 40 tangu kuanzishwa kwake, kimekuwa kikifanya uwekezaji mkubwa upande wa Tanzania Bara pekee. Pamoja na miradi hiyo iliyopo sasa hivi AICC bado ina malengo ya kujenga kituo kikubwa cha mikutano cha Mt. Kilimanjaro International Convention Center nyingine katika eneo la Jiji la Dodoma.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu mazingira ya uwekezaji kwa shughuli za AICC yaliyoko yanaruhusu, ni sababu zipi zilizofanya Wizara isifanye uwekezaji katika Visiwa vya Zanzibar? AICC kutowekeza Zanzibar ni kuwanyima Wazanzibari fursa za kiuchumi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Kutafuta Wawekezaji Nje ya Nchi. Miongoni mwa kazi ya Wizara ni kusimamia balozi zetu katika kutafuta wawekezaji, fursa za ajira, nafasi za masomo kwa bidhaa zetu. Wawekezaji wengi kutoka nje ya nchi wamekuwa wakija kuwekeza hapa nchini lakini kwa bahati mbaya wanaishia Tanzania Bara pekee. Ni kwa nini Wizara hii haiwaongozi wawekezaji kutoka nje kuwekeza katika visiwa vya Zanzibar kwa ajili ya kuimarisha uchumi wa visiwa hivyo ambao unadorora? Niombe Wizara isifanye upendeleo katika kufanya kazi zake.

Mheshimiwa Naibu Spika, Changamoto za Utawala Bora Zilizobainishwa na APRM. APRM inaamini kwamba Tanzania ina tatizo la kutozingatia utawala bora na unaokubalika kwa wananchi wake. Hii imetokana hasa pale Tanzania inapominya uhuru wa Wazanzibari wa kuiweka madarakani Serikali wanayoitaka wenyewe. Serikali ya Zanzibar iliyopo madarakani sasa hivi si chaguo la wananchi wa Zanzibar, ni Serikali iliyowekwa kwa nguvu za dola, hivyo basi Serikali hii si halali.

Mheshimiwa Naibu Spika, niombe tu Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itoe ripoti kwa APRM kwamba Tanzania haiwezi Mfumo wa Vyama Vingi kwa sababu Chama cha Mapinduzi hakiko tayari kukabidhi madaraka pale wanaposhindwa kwenye uchaguzi.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.