Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nichangie katika hoja hii kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Kurejesha Wafungwa Nchini; naomba Wizara ishughulikie kurudisha Watanzania waliofungwa huko nje, kama vile Msumbiji, warejeshwe nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, Wanajeshi Wanaofariki Kwenye Mapambano; kuna Wanajeshi wanaokwenda kusaidia nchi nyingine kwa ajili ya ulinzi kama vile Congo na sehemu nyingine, wanapofariki kwenye mapambano hayo familia zao zinasahaulika. Naiomba Serikali ihakikishe familia za Wanajeshi hao zinapata huduma stahiki.

Mheshimiwa Naibu Spika, Unyanyasaji wa Mabinti Wanaokwenda Kufanya Kazi za Majumbani Nje; naiomba Serikali ifuatilie wale wote wanaowasafirisha mabinti kwenda nje kufanya kazi za ndani, wachukuliwe hatua kwa sababu mabinti hao wanateseka sana na wengine wanakufa na hawapati masaada wowote.

Mheshimiwa Naibu Spika, Upungufu wa Maafisa Kwenye Balozi; Maafisa kwenye Balozi zetu hawatoshi. Naiomba Serikali ijitahidi kupeleka maafisa katika balozi zetu zote.

Mheshimiwa Naibu Spika, Viwanja Visivyoendelezwa. Kuna viwanja ambavyo havijaendelezwa basi viendelezwe.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.