Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Hon. Khadija Hassan Aboud

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

MHE. KHADIJA HASSAN ABOUD: Mheshimiwa Naibu Spika, naipongeza Wizara, Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri na watendaji wote wa Wizara, Mabalozi wetu wote wanaowakilisha Tanzania kwa jitihada kubwa ya kuitangaza nchi yetu pamoja na kuitafutia misaada mbalimbali kwa maendeleo ya nchi yetu na wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, michango na ushauri:-

Mheshimiwa Naibu Spika,Wizara hii ipelekewe fedha kwa wakati ili kutekeleza majukumu yake kwa muda muafaka. Pia fedha za maendeleo ziongezwe ili kutekeleza miradi mingi ambayo inahitajika kwa muda huu na baadaye kwa maslahi ya nchi yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni vyema Serikali ya Muungano ijenge jengo jipya la Ofisi ya Mambo ya Nje huko Zanzibar. Serikali iombe kiwanja kwa SMZ na ijenge jengo jipya na la kisasa kulingana na kazi na mahitaji husika.

Mheshimiwa Naibu Spika,Wizara iendelee na juhudi za kuwatafutia ajira vijana wa Tanzania nchi za nje na Taasisi nyingine za Kimataifa.

Mheshimiwa Naibu Spika, Watanzania waishio nchi za nje ambao wamepata mafanikio na maendeleo makubwa, wahamasishwe zaidi kuja kuwekeza nchini kwao Tanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, Balozi zetu ziongezewe fedha ili kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazojitokeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itenge fedha kwa madhumuni ya kufanyia matengenezo Balozi zetu nchi za nje.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante na naunga Mkono hoja. Nawatakia utekelezaji mwema wa majukumu ya kazi na kulitumikia Taifa.