Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Hon. Martha Moses Mlata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

MHE. MARTHA M. MLATA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kupata nafasi hii ya kutoa mchango wangu kwa njia ya maandishi katika Wizara hii. Naomba nianze kwa kumpongeza sana Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri kwa kazi nzuri sana wanayoifanya. Nampongeza Katibu Mkuu na Naibu wake na watendaji wote na Wakuu mbalimbali wa Idara zote zilizoko Wizarani.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimpongeze sana na kumshukuru Mheshimiwa Rais wetu Dkt. John Pombe Magufuli kwa dhamira yake ya dhati ya kutaka kuinua Taifa letu katika Diplomasia ya Uchumi na uhusiano mzuri na Mataifa mengine duniani kwa kuwapa nafasi wataalam wake kufanya kazi hiyo bila yeye kukanyaga katika nchi hizo.

Mheshimiwa Naibu Spika, hakika uamuzi wake wa kuwaamini na kuwapa nafasi wataalam wote wakiwepo Mabalozi wetu wote walioko nje ya nchi na waliopo ndani ya nchi. Uwezo wao wa uzalendo wao, tumeuona kwani mahusiano ya Taifa letu yamezidi kuwa mazuri na kuimarika, kiuchumi, kiusalama na kisiasa, ahsante sana Mheshimiwa Rais na hongera sana watendaji na Mabalozi wote.

Mheshimiwa Naibu Spika, natambua kazi kubwa sana inayofanywa na Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri, Katibu Mkuu na Naibu Katibu Mkuu ya kumwakilisha Mheshimiwa Rais kwenye mikutano mbalimbali na majukumu mbalimbali ya Kimataifa, huko nako hatujapungukiwa. Pia pongezi kwa Mabalozi ambao wao wako hapa Tanzania, lakini nchi nyingine ya kuibua mazuri yote kwenye Kanda wanazozisimamia mfano, Mabalozi wanaosimamia Idara mbalimbali kama; Mashirika ya Kimataifa, Kanda ya Afrika, Kanda ya Asia, Kanda ya Ulaya na Kanda ya Amerika.

Mheshimiwa Naibu Spika, nawapongeza sana hawa balozi wanaosimamia Kanda hizi. Kwani mambo yanaenda vizuri sana tumeona viongozi mbalimbali wakija nchini na wafanya biashara wengi wakija nchini kwetu, pongezi sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia naomba nipongeze utaratibu nzuri sana ambao Wizara imefanya wa kuleta vitabu ambavyo vina anwani za Balozi zote zilizoko nje ya nchi na ndani ya nchi yetu, pongezi sana. Pia kitabu kizuri cha utekelezaji wa diplomasia ya Tanzania kuelekea uchumi wa viwanda 2020. Utaratibu huu ni mzuri sana, naomba uendelee na ikiwezekana, angalau kuonyeshwe na moja ya fursa iliyoko katika nchi husika. Pongezi sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kutoa ushauri kuhusu nyumba na majengo ya baadhi ya Balozi zetu nje. Majengo haya yanatia doa nchi yetu kwa uchakavu. Naomba Waziri alipeleke shauri hili kwenye Baraza la Mawaziri ili jambo la bajeti ya kukarabati nyumba hizi lichukuliwe na Hazina, Wizara haitaweza bajeti yake ni ndogo. Mfano, nyumba za London niliwahi kwenda, haziridhishi. Naomba sana u-smart wa mtu humpa heshima kwa wanaomtazama. Hivyo, tunaweza tukadharaulika na Mataifa mengine kutokana tu na uchakavu wa majengo yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kumekuwa na utaratibu wa kubadilishana wafungwa, Je. Serikali inasemaje juu ya kuwarejesha Watanzania ambao wamehukumiwa kwa makosa mbalimbali duniani?

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo, naunga mkono hoja.