Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Dr. Adelardus Lubango Kilangi

Sex

Male

Party

Ex-Officio

Constituent

None

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa wasaa wa kuanza kuwa mchangiaji wa kwanza upande wa Serikali. Nitajielekeza moja kwa moja kwa hoja iliyoibuliwa na Mheshimiwa Nsanzugwanko (Mbunge), lakini pia alikuwa ananukuu Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii katika ukurasa wa 16 na 17 ambayo inahusu zoezi la kuhuisha vibali vya uwindaji ambapo Mheshimiwa alizungumza na iko hivyo katika taarifa kwamba Mheshimiwa Waziri alihuisha vibali hivyo mwezi Januari, 2017 lakini mwezi Oktoba akatoa tangazo la kuvifuta. Mwezi Disemba akatoa tena tangazo au maelekezo ya kuongeza kipindi cha miaka miwili kwa vibali hivyo. Kwa hiyo, maoni ya Kamati pamoja na Mheshimiwa Mbunge ni kwamba Mheshimiwa Waziri alivunja sheria, na kwa hiyo, akaomba mahsusi Mwanasheria Mkuu wa Serikali atoe position.

Mheshimiwa Spika, position ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali katika suala hili ni kwamba Mheshimiwa Waziri hakuvunja sheria. Mheshimiwa Waziri alipochukua hatua hizi na imeelezwa vizuri katika ile barua ya kwanza ya kuongeza muda ya mwezi Januari lakini pia na kwenye hayo mawasiliano mengine ya mwezi Oktoba na mwezi Disemba kwamba alikuwa anachukua hatua hizo kwa ajili ya kuweka mfumo mzuri zaidi wa uendeshaji wa vitalu kwa namna ambayo Taifa litaweza kufaidika zaidi kuliko hali ilivyo sasa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa nilikuwa napenda kukuthibitishia na kukuhakikishia na kumhakikishia Mheshimiwa Mjumbe pamoja na Kamati kwamba Mheshimiwa Waziri alipofanya hivyo alikuwa pia anatekeleza sheria.

Mheshimiwa Spika, swali litakuja ni sheria gani hii ambayo Mheshimiwa Waziri alikuwa anaitekeleza. Sasa nitaomba nilikumbushe Bunge lako tukufu kwamba mnamo mwaka jana mwezi wa saba Bunge hili lilitunga sheria na hii sheria inaitwa The Natural Wealth and Resources Permanent Sovereignty Act. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lengo kubwa la hiyo sheria ilipotungwa mwaka jana na Wabunge wote ni mashahidi nafikiri mijadala ilikuwa mikali na kadhalika, lakini ilikuwa zaidi kuhuisha Ibara za 9 na 27 za Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sehemu hii ya Katiba katika sheria tunasema inahitaji enabling law uweze kuitekeleza. Sasa nadhani ni vema nikarejea kwa ufupi na kwa haraka kabisa Ibara za 9 na 27 za Katiba zinasemaje. Nitakwenda Ibara ndogo (c) na Ibara ndogo (i) lakini nitakwenda zaidi (c) inatosha; kwamba shughuli za Serikali zinatekelezwa kwa njia ambazo zitahakikisha kwamba utajiri wa Taifa unaendelezwa, unahifadhiwa na unatumiwa kwa manufaa ya wananchi wote kwa jumla na pia kumzuia mtu mwingine kumnyonya mtu mwingine. Hiyo ni Ibara ya 9. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Ibara ya 27 inasema; watu wote watatakiwa na sheria kutunza vizuri mali ya mamlaka ya nchi na ya pamoja na kupiga vita aina zote za uharibifu na ubadhirifu na kuendesha uchumi wa Taifa kwa makini kama watu ambao ndio waamuzi wa hali ya baadae ya Taifa lao. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kama nilivyokwishasema palikuwa na matatizo katika suala zima la hivi vibali vya uwindaji na kwa hiyo Mheshimiwa Waziri akachukua hatua hizo kulingana na hii sheria mpya. Nafikiri niende pia kwenye hiyo sheria mpya ya The Natural Wealth and Resources Permanent Sovereignty inatuambia nini. Naomba niende kifungu cha 6(1) na ninaomba niirejee hapa kinasema; “It shall be unlawfully to make any arrangement or agreement for the extraction, exploitation or acquisition and use of natural wealth and resources except where the interest of the people of the United Republic are fully secured.” (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri aliongozwa na kifungu hicho, lakini kipo kifungu chenye nguvu zaidi ambacho actually kinampa maelekezo Waziri na hana jinsi nyingine. Kifungu cha 6(3) na chenyewe naomba nikisome; “It shall be the duty and responsibility of the Government. all organs and persons or authorities exercising executive, legislative or judicial functions to take cognizance of, observe and apply the provisions of this Act.”

Mheshimiwa Spika, kifungu hicho kinamfunga Waziri kwamba ni lazima ajue kwamba sheria hiyo ipo na kwa hiyo ni lazima chochote anachofanya kuanzia sheria ilipotungwa aongozwe na sheria hiyo.

Mheshimiwa Spika, sasa ninaelewa baada ya kusema hayo swali linaibuka je, kuna mgongano wa sheria. Position ya Mwanasheria Mkuu tena hapa katika swali hili ni kwamba hakuna mgongano wa sheria kwa sababu hii ni sheria msingi na umsingi wake unapatikana kwenye kifungu hicho nilichosema cha 6(3) kwa hiyo ina nguvu kuliko sheria nyingine. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, muda umekwisha nakushukuru sana.