Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Spika, nichukue fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Waziri na Naibu wake pamoja na watendaji wote. Narejea ukurasa wa 37 wa hotuba ya Waziri kuhusu matumizi ya mkaa. Nampongeza kwa kutambua umuhimu wa matumizi ya mkaa na kuja na mkakati mzuri. In short ingependeza zaidi kama elimu hii ya matumizi ya mkaa ingehusisha viongozi wote wa ngazi ya chini kama watendaji (VEOs/WEOs) ambao wana jukumu la kutoa elimu hiyo na ujumbe kufika kwa haraka. Kwa kuwa teknolojia hiyo ya gesi bado wananchi hawana uwezo wa ku-afford kununua gesi ni vizuri Serikali ikaendelea kuruhusu matumizi ya mkaa.

Mheshimiwa Spika, tunaomba Maafisa Maliasili na Utalii kwenye Halmashauri zetu ikiwemo Manispaa ya Singida kuwa na mpango kazi wa kuboresha eneo hili. Kwa mfano Singida tunavyo vyanzo vya utalii vingi ikiwa na fukwe. Niombe Serikali itoe maelekezo ya kila Halmashauri kupitia mikoa yao waandae na kuleta taarifa ya maliasili na utalii. Hii itasaidia kubaini maeneo hayo na kuongeza wigo wa utalii.