Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Daniel Edward Mtuka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. DANIEL E. MTUKA: Mheshimiwa Spika, nianze kuhusu migogoro ya mipaka baina ya hifadhi za wanyamapori/misitu na wananchi. Katika ya Jimbo la Manyoni Mashariki jumla ya vijiji 12 vimepakana na Hifadhi za Kizigo na Muhesi. Vijiji hivi ni Chikola, Chikombo, Mpola,
Iteka Azimio, Nkonko, Chidamsulu, Iseke, Mpapa, Simbanguru, Sasilo, Chisinjisa na Imalampaka.

Mheshimiwa Spika, wananchi katika vijiji tajwa hapo juu wanalalamikia uhaba wa ardhi kwa ajili ya kilimo, malisho ya mifugo, uchimbaji wa madini pamoja na ufugaji wa nyuki. Aidha, wanalalamikia kitendo cha kuzuiwa kutumia maji ya mto uliopo mpakani kati ya hifadhi na vijiji. Uhaba wa ardhi umejitokeza baada ya ardhi yao kuchukuliwa na Serikali ulipofanyika upanuzi wa mipaka ya hifadhi za misitu tajwa mwaka 1994.

Mheshimiwa Spika, Muhesi Game Reserve imeanzishwa rasmi kupitia GN Na. 531 ya tarehe 04/11/1991 na kusainiwa na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tarehe 09/03/1994. Muhesi ni hifadhi changa yenye kilometa za mraba 2000 na kwa hiyo imesababisha machungu makubwa kwa wananchi katika maeneo haya. Tangazo la kuipandisha Muhesi kuwa game reserve mipaka yake mipya imeleta madhara makubwa kiuchumi kwani imechukua maeneo muhimu kama eneo muhimu la kilimo cha mahindi liitwalo Chiumbo na eneo la machimbo ya dhahabu aina ya alluvial yaliyogunduliwa mwaka 1991. Hii ni dhahabu bora ambayo haijawahi kuonekana na kuchimbwa mahali pengine katika nchi hii (Ref: Taarifa ya Benki Kuu ya Tanzania, 1992).

Mheshimiwa Spika, maeneo au vitongoji vingine vilivyochukuliwa ni pamoja na Chosola, Msisi, Ilevelo, Machocholoni, Mkindilya, Chigugu, Ngongolelo pamoja na Chibwee. Aidha, maeneo haya yaliyochukuliwa yalitegemewa sana katika malisho ya mifugo, ufugaji wa nyuki na vyanzo vya maji safi ya kunywa binadamu na mifugo katika Mito ya Muhesi na Kizigo. Malalamiko mengine ni unyanyasaji utesaji na udhalilishaji vinavyofanywa na askari wa game reserve dhidi ya wananchi.

Mheshimiwa Spika, naambatisha na taarifa ya malalamiko ya wananchi yenye kichwa cha habari; “Yah: Malalamiko ya Wananchi Kuhusu Migogoro ya Mipaka Baina ya Vijiji 12 na Hifadhi za Muhesi na Kizigo; na Manyanyaso ya Askari wa Hifadhi Dhidi ya Wananchi.”

Mheshimiwa Spika, malalamiko haya yaliwasilishwa na wananchi 18 kutoka Jimbo la Manyoni Mashariki wakiongozwa na Mbunge wao Daniel Mtuka walipokutana kwa mazungumzo ya ana kwa ana ofisini kwao (Dodoma) Naibu Mawaziri wawili; kwa wakati huo walikuwa Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Engineer Ramo Makani, tarehe 27/05/2016 (mchana) na Naibu Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi Mheshimiwa William Tate Ole Nasha tarehe 27/05/2016 (mchana).

Mheshimiwa Spika, tunasikitika, hadi leo hatujibiwi (mwaka mzima)

Mheshimiwa Spika, ombi, wananchi wangu bado wanasubiri majibu.