Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Yosepher Ferdinand Komba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. YOSEPHER F. KOMBA: Mheshimiwa Spika, kwanza namshukuru Mungu kwa siku hii na nafasi ya kuchangia Wizara hii kwa maslahi ya Watanzania na wananchi wa Tanga. Katika Wilaya ya Muheza, Tarafa ya Amani kuna vivutio vizuri na vya asili vya utalii kama misitu mikubwa, maporomoko ya maji, vipepeo adimu duniani, kima na sokwe wa kipekee lakini pia katika Kata ya Magoroto kuna kivutio kikubwa cha mito na michikichi. Pamoja na vivutio vyote hivyo bado hakuna jitihada za makusudi kuvitangaza vivutio hivyo ili kuongeza watalii na pato la Taifa. Je, Wizara ina mkakati gani katika kufufua na kuvitangaza vivutio hivyo?

Mheshimiwa Spika, Mkoa wa Tanga na mikoa mingine ya Pwani imekuwa maarufu kwa mchezo wa bao ambao ni mchezo wa kipekee kwa jinsi unavyochezwa, na ni mchezo unaounganisha pamoja tamaduni za pwani kwa maana ya mavazi, ustaarabu wa dini hasa Waislamu. Naishauri Wizara iandae mkakati wa kuufanya mchezo huu unaoenzi tamaduni za watu wa Pwani ili uwe kivutio cha watalii wanapotembelea maeneo haya ya Pwani hasa fukwe na mapango kama ya Amboni.

Mheshimiwa Spika, katika Kata ya Mamba, Jimbo la Bumbuli vipo vijiji vilivyo karibu na Mbuga ya Mkomazi ambao wamekuwa wakisumbuliwa na wahifadhi wa Mkomazi Park na wamekataliwa kufanya shughuli za maendeleo katika makazi yao ambayo wameishi kwa miaka mingi tangu mababu zao. Je, Wizara ina mkakati gani wa kumaliza tatizo hili la mipaka ili wananchi waweze kuishi kwa amani katika maeneo yao na hifadhi ziendelee kuwa na faida kwa wananchi wanaozunguka hifadhi hizo.

Mheshimiwa Spika, naomba kupatiwa ufafanuzi.
Ahsante na nawasilisha.