Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Spika, Wizara hii ni muhimu sana endapo itazingatia ushauri wa Kamati, hususani katika suala la kutatua migogoro iliyopo kati ya wananchi na Hifadhi za Taifa (mipaka).

Mheshimiwa Spika, ni lini mtakuja Katavi kufuatilia na kutatua migogoro iliyowaathiri Wana Katavi hususani katika Kata za Isengule, Ikola, Kapala Msenga kijiji cha Lyamgoloka Jimbo la Mpanda Vijijini (Ikuba). Wananchi walipigwa na askari wa wanyamapori tangu 2004 mpaka sasa wananchi wanaishi kwa hofu, wanauawa kwa kupigwa risasi. Hivi karibuni kuna vijana wameuawa kwa kupigwa risasi.

Mheshimiwa Spika, akina mama wanabakwa, wananyang’anywa mali zao, je, Mheshimiwa Waziri ni sheria ipi inayoruhusu unyanyasaji huu kuendelea kutokea na Serikali hii inakaa kimya? Je, Serikali inasemaje kuhusu ukatili huu? Ni utaratibu gani unatumika kupima mipaka? Je, wananchi wanaingia ndani ya hifadhi au hifadhi inaongeza maeneo kwa kuwanyang’anya maeneo yao? Ni lini mtawalipa fidia kwa kuchukua maeneo yao bila utaratibu wa sheria?

Mheshimiwa Spika, mgogoro wa mpaka kati ya Stalike na hifadhi mpaka sasa wananchi hawa ni lini watarudishiwa maeneo yao? Wananchi wa kata hii wameshindwa kufanya shughuli za kiuchumi kulima na kutumia maji ya mito inayowazunguka. Je, ni lini jambo hili litaisha ili wananchi wafanye shughuli zao za kiuchumi?

Mheshimiwa Spika, kupigwa risasi ng’ombe/wafugaji; wafugaji wengi hawana elimu ya mipaka, makazi na hifadhi ni kwa nini elimu haitolewi kwa vijiji/vitongoji? Serikali ina kazi gani? Serikali kushindwa kuweka mipaka kumepelekea wafugaji kuendelea kunyanyasika katika Taifa lao.

Mheshimiwa Spika, sheria inasemaje kuhusu mauaji ya wafugaji na ng’ombe kupigwa risasi hovyo katika Kata za Ikuba, Majimoto, Luhagwe? Je, Serikali inasaidiaje tatizo hili la kitendo cha TANAPA kuvunja sheria kwa kuweka mipaka iliyo kinyume na GN.

Mheshimiwa Spika, suala la wafugaji kulipishwa faini na watendaji/askari wa wanyama pori ng’ombe mmoja inalipishwa shilingi milioni moja ikiingia hifadhi au mfugaji kupigwa risasi, Je, sheria ya haki za binadamu Wizara hii mbona iko kimya kuhusu unyama huu?

Mheshimiwa Spika, risiti fake wanazolipishwa wafugaji wetu je, Wizara inachukua hatua gani kuhusu tatizo hili? Ajira kupitia wawezeshaji hoteli zilizopo ndani ya hifadhi, Mkoa wa Katavi haunufaiki kwa wazawa kupata ajira mbugani, je, Serikali haioni ni tatizo?