Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Amb. Adadi Mohamed Rajabu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muheza

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja na ningependa kuchangia kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, nawapongeza kwa kazi kubwa mnayoifanya hususan katika sekta ya utalii. Nashauri mtumie vizuri ndege hizi ambazo zinakuja/zilizonunuliwa na Serikali kuongeza idadi ya watalii. Aidha, utumiaji wa Tour Operators zilizopo (ama zianzishwe) nje ya nchi ni muhimu zitumike.

Mheshimiwa Spika, eneo la Amani – Muheza ambalo Waheshimiwa Mawaziri wote mmefika ni eneo zuri ambalo linaweza kuwa kivutio kizuri kwa watalii. Naomba uliboreshe, kuna miti mirefu kuliko sehemu nyingi duniani, majoka makubwa, maua na kadhalika, kuna vipepeo ambao ni vivutio na pia ni biashara kwa wanakijiji wa Fanusi – Amani, ambao wanapeleka vipepeo hao nje kwa wingi.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo tangu Serikali ipige marufuku usafirishaji wa wanyama hai nje ya nchi wananchi wa Fanusi wameathirika. Mheshimiwa Waziri uliahidi kuboresha mazingara ya utunzaji wa vipepeo hao lakini bado wakala wa misitu amesahau naomba kukumbushia.

Mheshimiwa Spika, mgogoro wa watu 1,028 wa Derema bado haujamalizika. Tumeanza kuwapatia maeneo kwa kushirikiana na Wakala wa Misitu lakini bado kuna suala la upungufu wa fidia zao. Tumeongea jana na Naibu Waziri na Katibu Mkuu na naomba ulishughulikie.

Mheshimiwa Spika, miti ya tiki ambayo inalimwa Lunguza – Muheza bado tatizo la kuruhusu wakazi wa Muheza au wanunuzi kuwa na uwezo wa kushindana nadhani halijatatuliwa. Tunaomba utaratibu wa zamani (kwa maboresho kidogo) mgao wa wananchi urudishwe na waweze kupatiwa fursa ya kufunga viwanda vidogo vidogo hapo hapo Muheza badala ya matajiri wachache kununua vitalu vyote na kutoa miti hiyo nje ya Muheza.

Mheshimiwa Spika, lipo tatizo lingine kubwa dhidi ya Maafisa Misitu la utoaji wa vibali vya kukata miti hovyo. Kwa mfano Afisa Misitu wa Muheza juzi Baraza la Madiwani limearifiwa kukatwa mivule 100 nje ya utaratibu. Sasa pamoja na wazo la kuanzishwa Mamlaka ya Misitu lakini Maafisa Misitu pia wangehamishiwa chini ya Katibu Mkuu wa Wizara.