Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Naibu Spika, nachukua nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri kwa kazi nzuri wanazofanya. Wenye macho wanaziona, endeleeni, tuko pamoja, tunawaunga mkono.
Mheshimiwa Naibu Spika, mchango wangu utajikita katika maeneo yafuatayo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Mfuko wa Kuendeleza zao la Korosho (CDTF) unapokea fedha nyingi za Export Levy na sh. 10/= kwa kilo zinazochangwa na wakulima. Hata hivyo, Mfuko huu hauna uwazi na sehemu kubwa ya fedha zinatumika kwenye Administrative Expenses badala ya kuendeleza zao la korosho.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Waziri afuatilie matumizi ya fedha za Mfuko huu na kuhakikisha kuwa, kuwe na Menejimenti na Bodi ambayo ni “vibrant” na “aggressive.”
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali sasa iwe na mpango unaotekelezeka wa kubangua korosho na kuacha kuiuza korosho ghafi. Pia Serikali iwe na mkakati wa kuhamasisha ubanguaji mdogo kwa kutumia vikundi vya vijana na akinamama na Viwanda vya zamani vya Korosho vifufuliwe.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mkoa wa Mtwara una uzalishaji mkubwa wa zao la muhogo. Wakulima wengi wanaacha kulima kwa kukata tamaa ya kukosekana kwa soko la uhakika. Naomba Serikali iweke wazi kuhusu soko la muhogo. Kuna tetesi kuwa China wapo tayari kununua muhogo huu, naomba kauli ya Serikali kuhusu suala hili.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mkoa wa Mtwara unafaa kwa kilimo cha pamba, lakini Serikali iliweka zuio kwa kuhofia ugonjwa ambao ungeenea katika maeneo mengi. Je, itaondoa lini zuio hili ili hata Mtwara iendelee na mipango yake ya kuendeleza zao la pamba?
Mheshimiwa Naibu Spika, nawasilisha.