Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Ussi Salum Pondeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chumbuni

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. USSI SALUM PONDEZA AMJADI: Mheshimiwa Spika, kwanza naanza kwa kumshukuru Mungu kutujalia uhai na afya njema na hivyo kuweza kuhudhuria vikao vinavyoendelea vya Bunge letu hili.

Mheshimiwa Spika, naanza kwa kumpongeza Mheshimiwa Waziri kwa kazi nzuri anayofanya yeye na mtaalam wake, kwa jinsi wanavyofanya vizuri kwa muda aliokaa, kuna mambo mengi mazuri ambayo ameyafanya.

Mheshimiwa Spika, nampongeza kwa kanuni mpya alizozitunga kwa Wizara, zimeifanya Wizara yake ionekane jinsi gani inafanya kazi kwa maslahi mapana ya wanyonge. Nampongeza pia Mheshimiwa Waziri kwa kuanzisha (Tourism One Stop Centre) ambalo limejengwa jengo la mamlaka katika Mji wa Arusha.

Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa programu ya ujirani mwema kwa kuchangia miradi ya vijiji zaidi ya 30 vinavyozunguka hifadhi kwa kuwachimbia visima, zahanati, vyumba vya madarasa na mambo mengine. Changamoto pia haziko kuhusu mifugo inayoingia kwenye hifadhi, adhabu zake ni kweli zinahitaji kuboreshwa zaidi kwani utaratibu uliopo haukidhi kwani haijakaa vyema.

Mheshimiwa Spika, ushauri wangu, wanyama wanaoingia utaratibu ungekuwa Wizara kutoa mwongozo wa kuwa wale ambao mifugo yao imeingia kwenye hifadhi basi wao ndio wapewe kipaumbele ili kuondoa dhana ya rushwa kwenye zoezi hili.

Mheshimiwa Spika, mwisho nampongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri na watendaji wao jinsi wanavyofanya kazi vizuri.