Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Maftaha Abdallah Nachuma

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtwara Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA: Mheshimiwa Spika, ni kwa muda mrefu sasa Mikindani Mtwara kuna majengo mengi ya kale ambayo yangeweza kuvutia sana utalii Mtwara na Kusini kwa ujumla wake. Mtwara kwa kushirikiana na Trade Aid – Shirika la Charity kutoka Uingereza tuliweka Siku ya Mikindani ili kuutangaza rasmi Mji wa Mikindani kuwa ni mji wa utalii Tanzania na hasa katika sekta ya mali kale.

Mheshimiwa Spika, tulipanga kila kituo lakini Wizara kwa nini inasuasua kulifanya hili kwa maendeleo ya Mtwara, Kusini na nchi kwa ujumla wake? Naomba Wizara ituambie Wana Mtwara Mikindani lini watazindua Siku ya Mikindani ili kuutangaza utalii?

Mheshimiwa Spika, kuhusu fedha za Regrow; kuna fedha zaidi ya shilingi bilioni mbili za kuendeleza utalii kusini. Fedha hizi zimepelekwa Morogoro, Iringa ambako sio Kusini, Kusini kijiografia na kiutawala ni Mtwara na Lindi pamoja na Ruvuma. Mikoa hii imesahaulika sana pamoja na kuwa vivutio vingi vya kiutalii kwa nini fedha za Regrow Kusini zipelekwe maeneo mengine badala ya Kusini halisi?

Mheshimiwa Spika, kwa nini kila kinachopangwa Kusini kinahamishwa? Tatizo ni nini? Fedha za Regrow ziletwe Kusini Mtwara na Lindi ili ziendeleze Mikindani, Fukwe na Kilwa pamoja na Mbuga ya Selous upande wa Kusini.

Mheshimiwa Spika, Olduvai Gorge irudishiwe mali zake, hii ni mara yangu ya tatu naongelea hili. Eneo hili la mali kale lilikuwa linaingiza fedha sana kabla halijahamishwa kwa maslahi binafsi na kupelekwa Hifadhi ya Ngorongoro ambalo ni Shirika la Umma. Hivi sasa Olduvai Gorge inaingiza fedha ndogo sana kuliko wakati ikiwa mambo kale. Kama lengo ni kuongeza mapato, basi Olduvai Gorge irudishwe kwenye Idara ya Mambo Kale na si Ngorongoro.