Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Kabwe Zuberi Ruyagwa Zitto

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Kigoma Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. KABWE Z. R. ZITTO: Mheshimiwa Spika, makosa ya matumizi ya takwimu, ukurasa 73 aya 164; Wizara inasema mapato yatokanayo na utalii yameongezeka kutoka dola milioni 2.mpaka dola bilioni 2.25 mwaka 2016 – 2017. Kamati pia katika taarifa yake ukurasa 11 imerudia kusema; mapato yatokanayo na utalii mwaka 2016/2017 yameongezeka hadi dola bilioni 2.3; hili ni kosa. Dola bilioni 2.3 sio mapato ya sekta bali ni forex (fedha za kigeni zinazoingia kwenye reserve kutoka utalii). Tusichanganye forex na revenues. Matumizi ya takwimu hizi ni muhimu kutiliwa maanani. Tutumie mapato ya fedha za kigeni ili kuwa sahihi. Pia utalii unachangia 25% ya forex na sio 25% ya GDP.

Mheshimiwa Spika, mradi wa umeme Rufiji katika ukurasa 71 wakati wa mjadala wa makadirio ya Ofisi ya Makamu wa Rais, Mazingira, Serikali ilitoa commitment kuwa kabla ya mradi kuanza itafanyika ESIA. Hata hivyo TFS wametangaza zabuni ya kuvuna miti milioni mbili katika eneo lenye ukubwa sawa na Mkoa wa Dar es Salaam. Ni kweli kuwa hili eneo ni 3% tu ya Selous, lakini eneo husika ni eneo la mazalia ya wanyama. Kwa nini Serikali isisubiri ESIA iishe ili waanze utekelezaji? Kwa nini Serikali inafanya haraka hii?

Mheshimiwa Spika, narudia kusisitiza kuwa tutazame miradi mbadala iliyoainishwa kwenye Power System Master Plan (2016 update) ili kuepuka madhara ya mazingira katika Selous Game Reserve. Ni muhimu jambo hili tulitazame kitaifa ili kulinda maliasili zetu.

Mheshimiwa Spika, ni sahihi kuwa na uwezo mkubwa wa kuzalisha umeme lakini sio kwa kuharibu ekolojia. Kwa nini hatutumii bomba la gesi kikamilifu? Asilimia 25 ya bomba la gesi inazalisha umeme wote Stiegler’s. Kwa nini tuendelee na mradi huu?

Mheshimiwa Spika, nashauri ATCL wanahisa wake wawe TANAPA na NCAA. Hii ni kwa sababu wao ndio wafaidika wakuu wa Shirika la Ndege. Asilimia 15 ya makato yanayokwenda Hazina zitumike kama mtaji kwa ATCL.

Mheshimiwa Spika, suala la Loliondo lipate suluhisho ya kudumu kwani wananchi wanaumia sana. Mwaka 2017 boma 250 zilibomolewa na wananchi kupigwa sana. Waziri aliahidi kuwa OBC itanyang’anywa leseni ifikapo Januari, 2018. Hata hivyo mpaka leo OBC bado wapo. Kwa nini tusifuate sheria na kuiacha Loliondo kama village land?

Mheshimiwa Spika, CAG, ametoa hoja ya ukaguzi kuwa TANAPA na NCAA hukatwa mchango kwenye Mfuko Mkuu wa Hazina asilimia 15 na wakati huo huo kukatwa kodi asilimia 30 bila kuondoa makato yanayotambuliwa (allowance expense). Suala hili ni kinyume kabisa na principles za kodi kwani hiyo asilimia 15 ilipaswa kuondolewa kabla ya kutoza kodi. Ni muhimu sana Serikali ifuate ushauri wa CAG wa kurekebisha sheria ili kuwezesha makato yanayokwenda mfuko wa Hazina (Rejea CAG Pg. 98 – 99).