Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Joyce Bitta Sokombi

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. JOYCE B. SOKOMBI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kupata nafasi hii na mimi niweze kuchangia Wizara hii.

Mheshimiwa Spika, nitaanza na ukamataji hovyo wa wauza mikaa. Naomba utambue kuwa mkaa ni kimbilio la wananchi kwa 95% mfano mwananchi wa Kaburabura, Bugoji, Salagana, Kangetutya umwambie atumie gesi ni kichekesho cha hali ya juu.

Mheshimiwa Spika, kwanza vile usafirishaji wa gesi kutoka Mjini Musoma hadi ifike kusambazwa kwa wananchi huko vijijini ambako bado wanaamini kupika kwa kutumia kuni na mkaa, leo hii wananchi hao wananyanyasika kutokana na upatikanaji wa kupatikana (upatikanaji wa kuni) kwa kuni na mkaa.

Mheshimiwa Spika, Serikali inatakiwa iwasaidie wananchi wake na siyo kuwanyanyasa kwa sababu leo hii mtu akikamatwa hata na gunia moja la mkaa ni shida na linaweza kumfunga. Serikali inazuia ukataji miti hovyo sasa kama mnawazuia wananchi hata kupata kuni mnategemea mwananchi wa kijijini atapika kwa kutumia nini? Kwani wale watendaji wenu wananyanyasa wananchi kule vijijini kwani hata mwananchi akikamatwa na mzigo wa kuni au gogo lililoanguka lenyewe anashtakiwa na viongozi wa eneo husika eti kwa nini hajachukua kibali.

Mheshimiwa Spika, niiombe Serikali irekebishe kanuni zinazosimamia matumizi ya nishati ya mkaa kwani wananchi wengi wa vijijini hawajapata nishati mbadala ya kutumia kuni na mkaa.

Mheshimiwa Spika, Hifadhi ya Msitu wa Kyanyari uko chini ya TFS, mpaka sasa katika Kijiji cha Nyamikoma, Mwibagi Kata ya Kyanyari, Butiama kuna wananchi walifukuzwa ili kupisha eneo la msitu lakini toka walivyofukuzwa hadi leo wananchi hao bado wananyanyasika kwani hawana makazi maalum na mashamba.

Mheshimiwa Spika, wananchi wa Kyanyari wanateseka sana kwa kukosa maeneo ya kulima, niishauri Serikali kabla ya kufanya uhamisho kwa wananchi ili wapishe hifadhi ni vizuri iwaandalie maeneo kabla ya kuwahamisha ili wananchi wanapofurushwa wawe na eneo la kuweka makazi ya kudumu ya uhakika na sehemu ya mashamba ambapo wananchi watakuwa na uhakika wa kulima na kupata mazao ya chakula na biashara ili kuweza kukidhi mahitaji ya wananchi ya kila siku.