Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Eng. Gerson Hosea Lwenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. ENG. GERSON H. LWENGE: Mheshimiwa Spika, awali ya yote naunga mkono hoja kwa sababu naamini malalamiko ya wananchi wa Wilaya ya Wanging’ombe yaliyo na Pori la Akiba la Mpanga – Kipengere litafanyiwa kazi na Waziri.

Mheshimiwa Spika, kwenye hotuba ya Waziri ukurasa 69 imeelezwa kuwa Wizara inaweka beacons upya kwa kushirikiana na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, TAMISEMI na wananchi.

Mheshimiwa Spika, ushirikishwaji wa kazi hiyo haupo kwenye Pori la Akiba la Mpanga – Kipengere na taarifa hii nimemwambia Waziri na Naibu Waziri wa Wizara hii lakini hakuna hatua iliyochukuliwa TANAPA, bado TANAPA wameendelea kuweka beacons ndani ya vijiji vilivyoandikishwa kisheria. Jambo hili limeleta adha kubwa kwa wananchi hasa vijiji vya Iyayi, Igandu Hanganani, Ludwega, Mpanga, Malangali, Wangamiho, Masage na kadhalika. Naomba zoezi hili lisimamishwe ili ushirikishwaji wa kutambua mipaka ya awali iweze kutambuliwa ili kuondoa hofu kwa wananchi kwenye Serikali yao.

Mheshimiwa Spika, iliwahi kutolewa kauli ya Serikali katika kuondoa migogoro ya mipaka kuwa kuna Kamati ya Wizara ya Ardhi, Maliasili na TAMISEMI inayopitia kila hifadhi au Pori la Akiba zote nchini ili kutatua matatizo ya mipaka na vijiji vilivyoandikishwa na kuwekewa GN. Kazi hiyo sasa ni miaka mitatu sijawaona wakipita katika pori hili la Mpunga – Kipengere na hivyo kusababisha mgogoro huu kuwa mkubwa zaidi na kufanya wananchi wa jimbo langu kurudi nyuma katika kufanya kazi za maendeleo kwenye maeneo yao kwa kujenga mashule, zahanati na kilimo.

Mheshimiwa Spika, naomba Wizara hii iangalie upya haja ya kuwa na Mapori ya Akiba kwenye maeneo wananchi wameongezeka sana na itafika muda wananchi watakosa ardhi ya kuishi.