Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Spika, mipaka inayozunguka hifadhi ipitiwe upya. Kulingana na idadi ya watu kuongezeka nchini kumekuwa na muingiliano mkubwa sana kati ya wananchi na wanyama na kupelekea mahusiano mabaya kati ya wananchi wanaozunguka hifadhi na watumishi wanaohusika na kuhifadhi wanyamapori. Nashauri Serikali kupitia upya mipaka yake ili kuondoa migogoro isiyokuwa ya lazima.

Mheshimiwa Spika, sheria ya fidia ibadilishwe, suala hili limekuwa na malalamiko makubwa kwa wananchi pale inapotokea mtu au watu kuuawa, kujeruhiwa au mazao, makazi ya wananchi kuharibiwa, fidia au kifuta jasho haviendani na adhabu inayotolewa kwa mtu au watu wanapokamatwa wakiwa wameua mnyama au wanyama.

Mheshimiwa Spika, kuwekwe mazingira rafiki kwa wawekezaji, kumekuwa na changamoto za wawekezaji waliopo na wanaotaka kuja kuwekeza nchini kwetu. Kwa kuwa Taifa letu tunategemea utalii kukusanya na kupata pesa za kigeni ni vema kama Wizara kukawekwa mkakati wa makusudi utakaokuwa rafiki kwa wawekezaji wanaotaka kuwekeza kuja.

Mheshimiwa Spika, tozo na malipo kwa watalii ziangaliwe upya ili kuleta tija kwa Taifa letu kwa kuangalia tozo zote zenye kero ambazo zinaweza kufanya watalii wetu wakaweza kushindwa kuja kutalii na kusababisha Taifa letu kukosa mapato na kupeleka nchi nyingine.

Mheshimiwa Spika, suala la ugawaji vitalu, kumekuwa na malalamiko mengi kwa wananchi wanapokuwa wanataka kumiliki vitalu kwa kufuata taratibu na sheria tulizojiwekea, kumekuwa na ukiritimba mkubwa na kupelekea mianya ya rushwa na kufanya waone kuwa wageni wanapewa nafasi kubwa kuliko wageni wenyeji.

Mheshimiwa Spika, huduma za kijamii ziboreshwe kwa vijiji vinavyozunguka au karibu na hifadhi. Kumekuwa na changamoto kwa wananchi wanazunguka hifadhi ili kulinda wanyama hasa pale ambapo wananchi wanafuata huduma za maji na vitoweo mbali. Nashauri Wizara kuweka utaratibu mbadala wanapoona kuna umuhimu wa kufanya hivyo.

Mheshimiwa Spika, Wizara itoe elimu kwa maeneo yanayokuwa karibu na hifadhi ili kujua umuhimu wa uhifadhi na wao wananchi wajue kuwa wao ni walinzi wa kwanza kuliko ilivyo sasa wanavyojiona kama wanyonge.

Mheshimiwa Spika, Wizara ya Ardhi, Wizara ya Mazingira na Wizara ya Maliasili na Utalii kuna umuhimu wa kukaa pamoja ili kupitia suala la mipaka na shughuli za binadamu, kwa kuwa Serikali ni moja endapo kama mtakaa pamoja mtamaliza tatizo hilo kwa umakini.

Mheshimiwa Spika, utaratibu wa kubadilisha kutangaza vivutio vyetu ubadilishwe kwani utaratibu unaotumika kwa sasa haujaleta matokeo makubwa na ya haraka kwa Taifa letu kulingana na faida wanazozipata nchi nyingine zinazotuzunguka.