Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Nuru Awadh Bafadhili

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. NURU A. BAFADHILI: Mheshimiwa Spika, awali ya yote nimshukuru Mwenyenzi Mungu kwa kupata muda wa kutoa mawazo yangu kwa faida ya Watanzania.

Mheshimiwa Spika, mchango wangu wa kwanza nitajikita katika suala zima la utalii. Utalii ni sekta ambayo inalipatia faida Taifa letu. Mbuga nyingi zinazotangazwa ni Mikumi, Serengeti, Ngorongoro, Manyara na Selous. Mbuga hizi ndizo ambazo kila leo utasikia zikitangazwa katika vyombo vyetu mbalimbali vya habari. Kuna mbuga ya Saadani katika Wilaya ya Pangani, mbuga hii imepakana na ufukwe wa bahari. Katika maajabu ya mbuga hii utakuta simba na tembo na wanyama wengine wanacheza pamoja katika ufukwe wa bahari hivyo nayo ni maajabu.

Mheshimiwa Spika, ukiacha huo utalii wa wanyama pia kuna eneo katika Wilaya ya Tanga ambapo kuna maji moto yenye sulphur ambayo wenye matatizo ya ugonjwa wa upele huenda kuogelea hapo. Sehemu hiyo huitwa Amboni, Kata ya Mzizima Wilaya ya Tanga, eneo hilo ni maarufu kwa jina la Amboni Sulphur Baths.

Mheshimiwa Spika, katika vivutio vya utalii pia kuna sehemu katika Bandari ya Jiji la Tanga kuna eneo linaitwa Jambe, eneo hili kuna magofu ya mahandaki ambayo zamani watu walioishi hapo walitumia kujificha na pia kuna visima vilivyochimbwa na wenyeji walioishi wakati huo.