Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Spika, hoteli za kitalii na uhudumiaji wageni, ningependa kushauri Serikali kuanzisha vyuo maalum kwa ajili ya vyuo vya kuelimisha wahudumu wa kuhudumia watalii. Imekuwa watalii wengi wakilalamikia huduma zinazotolewa hapa nchini kuwa ni za chini sana.

Mheshimiwa Spika, hata waongozaji wa watalii ni kwamba hawana mafunzo maalum hivyo kuwa shida kwa watalii wetu. Gharama za juu kwa watalii hivyo kupunguza ujio wa watalii, mfano watalii kulipia huduma moja mara mbili kuliko ilivyo sasa ambapo mtalii analipia hoteli, analipia usafiri halafu anapofika kwenye eneo la mbuga anakutana na tozo ya kuingiza chombo hicho kwenye mbuga hii inakatisha tamaa kwa watalii.

Mheshimiwa Spika, nishauri gharama zinazolipwa wenye mahoteli hata kama watalii hawajalala hivyo kukatisha tamaa kwa wamiliki wa mahoteli ya kitalii.

Mheshimiwa Spika, vitalu vya uwindaji; nashauri Serikali kugawa vitalu kwa kuzingatia wazawa pia ugawaji wa vitalu uende kwa wakati. Pia nashauri kuwawekea mazingira mazuri ya uwekezaji katika utalii. Pia niishauri Serikali kuangalia upya juu ya mipaka ya kuhifadhi maliasili na mbuga kwa ujumla. Pia Serikali ihakikishe maeneo hayo ili yale ambayo hayatumiki yarudi kwa wananchi na yabadilishwe matumizi.

Mheshimiwa Spika, niishauri Serikali kuhakikisha inaongeza fidia kwa wananchi wanaopata madhara ya kuvamiwa na wanyama hivyo kuleta hasara kwa wananchi. Vikundi vya wanawake, wanawake wachonga vinyago mfano pale Mwenge. Niishauri Serikali kuyaangalia makundi haya ya wanawake wanaojishughulisha na vinyago wanawauzia watalii wetu wapewe mikopo ya kuwawezesha kutoka maliasili kuwasaida. Pia Serikali isaidie masoko ya vinyago.