Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Spika, naomba nichangie katika hoja hii kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kuhusu migogoro ya mipaka, kumekuwa na migogoro ya mipaka kati ya TANAPA na wananchi wa Kijiji cha Luduga katika Wilaya ya Wanging’ombe, Mkoa wa Njombe. Pia huko Kituro, Wilaya ya Makete, Mkoa wa Njombe wananchi wamekuwa wakisumbuliwa na TANAPA, kutokana na kuweka beacon kwenye maeneo yao ambayo hapo awali hayakuwa kwenye eneo la hifadhi lakini Serikali imeongoza. Hii imesababisha kuwavurugu wananchi wanaoishi maeneo ya mipaka ya hifadhi.

Mheshimiwa Spika, naiomba Serikali isitishe zoezi hili la kuweka mipaka hadi wawashirikishe wananchi katika maamuzi ya Serikali yanayohusu kuongezeka kwa maeneo ya hifadhi.

Mheshimiwa Spika, kutopeleka fedha kwa wakati naomba kujua ni kwa nini fedha hazipelekwi kwa wakati. Lakini pia kutopelekwa fedha zote zilizoidhinishwa na Bunge, lakini kwa wakati.

Mheshimiwa Spika, kumekuwa na tozo nyingi kwenye sekta ya utalii, matokeo yake kumesababisha kupunguza watalii wanaokuja nchini kwetu. Naiomba Serikali ipunguze tozo zisizo za muhimu.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.