Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Ester Alexander Mahawe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. ESTER A. MAHAWE: Mheshimiwa Spika, naomba kutumia fursa hii kutoa maoni yangu kwa Wizara hii ya Maliasili na Utalii. Utalii unachangia pato la Taifa kwa asilimia 17.5 lakini changamoto za Wizara hii kutokuuza pato hilo kama zilivyo nchi jirani kazi zinazotuzunguka ni nyingi mno, kati ya hizo naomba nitaje zifuatazo:-

Mheshimiwa Spika, bado hatujatenga bajeti inayotosheleza Wizara hii kufanya (marketing) matangazo ya kutosha kwa ajili ya ufinyu wa bajeti. Tanzania ni nchi pekee katika Ukanda wa Afrika Mashariki yenye vivutio vingi na visivyopatikana maeneo mengine lakini nchi hizo kama Kenya, Uganda, Rwanda na na kadhalika kutenga bajeti kubwa ya matangazo ya hifadhi na maliasili zao na hivyo kupata fedha nyingi zinazochangia chumi zao.

Mheshimiwa Spika, naomba kuishauri Serikali yangu iweze kuongeza bajeti ya Wizara hii ili tuweze kupata watalii wengi na tupate kuongeza fedha za kigeni.

Mheshimiwa Spika, nitoe masikitiko yangu kuhusu suala la single entry katika hifadhi hasa Ngorongoro na Serengeti. Huko nyuma wageni waliingia katika hifadhi na kutoka kwenda kwenye vijiji vya jirani kwa ajili ya kula, kunywa na pengine kuleta hali iliyofanya vijiji vya jirani kupata mapato ikiwa pamoja na kuongeza pato la mtu mmoja mmoja. Leo hii wakazi wengi wamebakia kuwa maskini na wengine wamekuwa vibaka. Kwa kukosa ajira walizokuwa wakizipata kupitia watalii hao.

Mheshimiwa Spika, ni ajabu sana na utashangaa kuacha system ya zamani na kuanzisha single entry eti ni kwa sababu tu mgeni anaweza kutoka na permit yake ikatumika na mtu mwingine, sababu hii inasikitisha kama nchi ina wataalam na wanaishi katika dunia yenye teknolijia kubwa kiasi hiki wanashindwa kujua yupi kaingia na yupi katoka, ndiyo mtalii yule yule? Ni ajabu sana.

Mheshimiwa Spika, kuna tozo na kodi lukuki ambazo zinazokatisha tamaa watalii wengine kutokuja Tanzania. Kodi hizi pia zimekuwa kero kwa wafanyabiashara wa utalii hasa tour operators na watu wa mahoteli. Naomba nishauri Serikali ikae na wadau wa utalii na ione ni kwa jinsi gani wanaweza kuondokana na kero ambazo si za lazima zinazokatisha tamaa wawekezaji hawa.

Mheshimiwa Spika, kwa nini tusiige kutoka kwa nchi kama Dubai na nyinginezo ambazo unakuta wanachaji viza ya dola za Marekani 150 tu ili kuvutia watalii wengi kuja huku kwetu? Watalii hawa wakija wanalala, wanakula, wanatembelea mbuga na kadhalika na kwa vyovyote vile lazima watuachie fedha nyingi za kigeni, kwani tunawakatisha tamaa kwa kuwawekea tozo nyingi zisizo na maana.

Mheshimiwa Spika, naomba Wizara hii ikae na wataalam na ione mbinu mbadala kwa kuongeza idadi ya watalii kutoka idadi ya watalii milioni 1.3 haidhuru mpaka milioni tatu. Mimi najua tunaweza na ninawaombee Mawaziri wetu, wataalam na watendaji wa Wizara hii kwa Mwenyenzi Mungu ili waweze kutekeleza majukumu yao ipasavyo.

Mheshimiwa Spika, naomba kuunga hoja mkono.