Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Bhagwanji Maganlal Meisuria

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chwaka

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. BHAGWANJI M. MEISURIA: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kushukuru Kiti chako kwa nafasi hii ya kuchangia kwa maandishi katika Wizara hii ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia napenda kumpongeza Rais wetu Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kwa kazi nzuri anayoifanya ya kujenga Taifa hili kwa falsafa ya “Hapa Kazi Tu” na kwa kweli tunaona kazi inafanyika kweli kweli na wananchi walio wengi wana imani na Serikali ya CCM.
Mheshimiwa Naibu Spika, nitakuwa mchoyo wa fadhila nisipompongeza Mheshimiwa Waziri Mkuu wa Tanzania kwa kumsaidia Rais wa Tanzania kutekeleza majukumu ya Serikali na sasa tunaanza kuona matunda yake.
Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho, nampongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Dkt. Ali Mohamed Shein kwa ushindi mkubwa alioupata hivi karibuni.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nichangie hotuba ya Wizara hii ya Kilimo kwa kuzungumzia mambo machache. Napenda kuishauri Serikali kuweza kuwakusanya vijana wasio na ajira na kuwatengea maeneo maalum ya mashamba na kupewa taaluma ya mifugo, uvuvi na Kilimo na baadaye wapewe mikopo kutoka Benki ili waweze kujiajiri wenyewe.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia naiomba Serikali kujipanga vizuri katika kukabiliana na changamoto zifuatazo:-
(a) Uharibifu mkubwa wa mazingira ya Bahari, Mito na Maziwa; na
(b) Kukabiliana na migogoro mikubwa ya wafugaji.
Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.