Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Deogratias Francis Ngalawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. DEOGRATIAS F. NGALAWA: Mheshimiwa Spika, Serikali iangalie uwezekano wa kuboresha maeneo ya mwambao wa Ziwa Nyasa inayozunguka na milima mizuri ya Livingistone. Maeneo haya yanafaa sana kwa utalii kwa sababu ya beach nzuri zilizopo mwambao wa Ziwa Nyasa. Katika eneo la Kata ya Lumbila, Tarafa ya Mwambao palijengwa boma la Mjerumani ambalo limezama ndani ya Ziwa Nyasa na Wajerumani kuhamisha boma hilo kule Tukuyu. Boma la Mjerumani la Tukuyu asili yake ni Lumbila. Kwa hiyo, Serikali ione uwezekano wa kuweka kumbukumbu kihistoria kwani historia hiyo haifahamiki. Maeneo haya yakipewa usimamizi na kushirikiana na wananchi tutapata maeneo mazuri na mengi ya kihistoria. Maeneo haya bado yana picha nyingi za kihistoria ambazo zimehifadhiwa hasa katika makanisa ya Katoliki, kuna historia nzuri sana.

Mheshimiwa Spika, eneo kubwa la Wilaya ya Ludewa ina vijito vya maji vinavyotiririka toka Milima ya Livingstone kuelekea Ziwa Nyasa. Vijito hivi baadhi vinatoka umbali wa kilometa 200. Hivyo kufanya maeneo mengi kuwa kijani (greenish) muda wote wa mwaka na kufanya mandhari nzuri ya maliasili ya nchi hii. Ifike wakati Serikali iwe na mkakati wa makusudi wa kutenga fedha za uhifadhi.

Mheshimiwa Spika, kuna haja ya Wizara hii ya Maliasili na Utalii kushirikiana na Wizara nyingine kama miundombinu na ulinzi ili kufanikisha utalii kuweza kufanyika katika maeneo ya kando kando ya Ziwa Nyasa. Kuna wageni wengi toka nchi mbalimbali hasa za Ulaya kutembelea maeneo haya hasa yaliyokaliwa na wageni Wamisionari. Wageni hawa wanapokuja wanakumbana na mazingira magumu hasa miundombinu ya barabara na mawasiliano.

Mheshimiwa Spika, tamaduni zetu hasa ngoma za asili zimeendelea kufifia mwaka hadi mwaka kutokana na kutopewa kipaumbele kikubwa. Kufifia kwa tamaduni hizi kumepelekea kumomonyoka kwa kiasi kikubwa kwa maadili ya vijana na watoto wetu. Lazima kuwe na mkakati wa moja kwa moja wa kuhamasisha watu kupenda tamaduni za makabila yetu. Viwepo vipindi maalum vingi vya ngoma zetu na pia kuwe na muda maalum hasa kuanzia baada ya shughuli za kilimo katika maeneo ya vijijini. Ni vizuri walau kwa mwaka mara moja katika vijiji vyetu. Ngoma hizi zinazohusha akina baba, akina mama na watoto kujenga mahusiano baina yao toka katika maeneo mbalimbali, hamasa iende maeneo mbalimbali hasa mashuleni sherehe na mengineyo.