Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Spika, vivutio vya utalii visivyotambuliwa na hivyo kutangazwa; kuna vivutio vingi sana katika visiwa vya Ukerewe ambavyo vikitambuliwa na kutangazwa vinaweza kuingizia Taifa pesa nyingi sana, miongoni mwa vivutio hivi ni:-

(a) Jiwe linalocheza Kisiwani Ukara katika Wilaya ya Ukerewe;
(b) Mapango ya Handebezyo;
(c) Makazi/Majengo ya Chifu Lukumbuzya; na
(d) Fukwe za kipekee maeneo ya Rubya na kadhalika.

Mheshimiwa Spika, hivyo Wizara ione umuhimu wa kutambua vivutio hivi, kuvijengea mazingira mazuri na kuvitangaza ili viweze kuliingizia Taifa mapato.