Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Joseph Leonard Haule

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mikumi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. JOSEPH L. HAULE: Mheshimiwa Spika, nianze na suala la migogoro isiyokwisha kati ya Hifadhi ya Mikumi na Vijiji vinavyopakana na hifadhi.

Mheshimiwa Spika, jana tu kumetokea mauaji ya vijana wawili katika Kijiji cha Ilakala kilichopo kwenye Kata ya Jimbo la Mikumi. Huu ni muendelezo tu wa mauaji ya watu wetu wengi katika Jimbo la Mikumi. Tunaiomba sana Serikali iweze kuingilia kati na kutoa adhabu kwa wahusika ambao wanasababisha mahusiano mabaya kati ya hifadhi zetu na vijiji vinavyopakana na kusababisha migogoro ya muda mrefu sana.

Mheshimiwa Spika, tembo wamekuwa kero sana katika Vijiji vya Kilangali, Mhenda, Mululu na kadhalika na kusababisha uharibifu mkubwa sana wa mazao, mali na hata watu kupoteza maisha. Njia hii inayotumiwa na Serikali ya Awamu ya Pili imeshindwa kabisa kwa kiasi kikubwa kusaidia kudhibiti tembo hao. Tunaomba sana Serikali ianzishe vituo vyenye askari katika maeneo haya muhimu ili waweze kusaidia kudhibiti tembo hawa ambao wanaleta madhara makubwa sana kwa wananchi wetu.