Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Gibson Blasius Meiseyeki

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Arumeru-Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. GIBSON B. MEISEYEKI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana, labda ni-declare interest kwamba ni mfanyabiashara wa utalii takribani miaka 20 sasa.

Mheshimiwa Spika, sitatofautiana na wengi ambao wamenitangulia kwa maeneo mengi niseme wameni-pre- empt some how. Lakini niseme idadi ya watalii tunayoipata nchi hii ni ya kusikitisha sana. Ni watalii wachache sana ukilinganisha na uzuri na natural gift ambayo tumeijaliwa kama Taifa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nasema ni wachache kwa sababu kuna nchi kama Thailand ambayo haina kabisa vivutio ambao naweza kusema wana robo tu ya tulichonacho sisi. Wao wanapata watalii milioni 35 kwa mwaka na wanaongezeko la watalii milioni moja na nusu kila mwaka. Sisi ongezeko letu ni tena kwa namba ya kuchakachua maana yake Mheshimiwa Dkt. Chegeni hapa amenigusa mahali. Kila siku tunaambiwa hapa tunaambiwa hapa imeongezeka lakini kiukweli mahoteli yetu yanalala bila wageni. Sasa tunashindwa kuelewa hawa wageni wanaoongezeka huwa wanakwenda kulala wapi. Sasa wanaongezeka angalau kwa namba hizi za kuchakachukua 100,000 kwa mwaka. Kwa hiyo, ili tuweze kufika watalii milioni tatu kwa mwaka tunahitaji miaka at least 15. Thailand kila mwaka wanaongezeko la watalii milioni moja na nusu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ulinifurahisha sana juzi uliposema kwamba hatuwezi kuwa na Mawaziri ambao wanakaa tu humu bila kwenda nje kujifunza. Basi kama kuna mmoja ambaye anatakiwa ahamie huko ili akajifunze kweli kweli sio kutalii kwenda kujifunza kweli kweli ili tujue kwa nini Thailand wao kwa miaka kumi wameongeza watalii zaidi ya milioni 15. Sisi tunahitaji miaka 15 ili kuongeza watalii milioni moja na nusu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, kiukweli tuwapigie chepuo hawa wakajifunze, Thailand wanafanyaje mpaka wapata watalii kiasi hicho. Sisi na uzuri wote huu tumezidi kulia lia tu na hii nchi tumekuwa wa ajabu sana kila mahali tunalia, kila sekta tunalia, wakulima wanalia, wavuvi wanalia kama watu walivyosema hapa na sisi humu Bungeni tunalia. Sasa mpaka wakati mwingine tunashindwa.

Mheshimiwa Spika tusaidie kama kuna kitu tunaweza kufanya ili hivi vilio vipungue kwenye nchi hii basi tufanyeni kama Wabunge kwa sababu kulia kumezidi. Unda, wamesema watu hapa hizi sekta zote ambazo zinamatatizo ambao Wabunge wengi tumekubaliana humu ndani ikiwezekana unda tume mbalimbali ili tufanye kazi yetu kama Wabunge tuunde tume mbalimbali kwa kila Idara ambayo tumeona kwamba tumekubaliana humu ndani ili ukafanyike upembuzi yakinifu na tuje hapa na maamuzi ya Kibunge ili kulia lia kuishe humu ndani ya hii nyumba, tunalia tu toka mwaka juzi. Kwenye Wizara hii ya Maliasili kwa miaka mitatu mfululizo tumekuwa tukilia hivi hivi na inaelekea tutaendelea kulia mpaka mwisho wa maisha yetu ni kulia tu humu ndani. Ifike mahali tuchore mstari, maamuzi yafanyike ili tuone kama yanaweza kuleta mabadiliko yoyote. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, Mheshimiwa Kigwangalla na wenzake pengine na Wabunge humu ndani iundwe tume tukaifanyie ovehaul hii idara ya Utalii ili tuweze kufaidika maanake utalii huu unaweza kutumalizia shida nyingi sana katika Taifa hili.

Mheshimiwa Spika, kwa sababu ya muda nimwombe Mheshimiwa Waziri sasa nilishamwomba Waziri aliyekuweko hapo kabla kwamba mwaka jana mwanzoni mliweza kuwapiga watu wangu watano risasi mkawaua na wengine zaidi ya nane kujeruhiwa na mmojawapo ni mtoto ambaye amepata ulemavu wa kudumu.

Mheshimiwa Spika, watu hawa toka wameuawa baada ya msaada wa mazishi hamjaenda kwenda tena kuwaona wala hakuna kifuta machozi. Kwa hiyo, nikuombe Mheshimiwa Waziri ukawaone watu wale na uwafute machozi ikiwezeka na tukio hilo lisirudie tena kwa sababu kwa kweli hali ilikuwa ni tete wakati ule. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hayo machache nashukuru sana.