Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Omary Tebweta Mgumba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. OMARY T. MGUMBA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuchangia Wizara hii muhimu ambayo iko kwa ajili ya maslahi ya Taifa letu. Tunafahamu kazi moja ya Bunge ni kutunga sheria, pamoja na kazi nyingine, lakini nikuombe ili Bunge lako liingie kwenye historia. Wakati mwingine tusiwe tunatunga sheria tu, wakati mwingine ije sheria tuzifute zile sheria ambazo zinakinzana na maslahi ya Watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa sababu misingi ya sheria iko mitatu, kuna sheria ya katazo, kuna sheria wezeshi, kuna sheria ongozi. Sheria katazo zile sheria zinakataza katakata usifanye jambo hilo, lakini sheria wezeshi ni zile ambazo tunazitunga kwa ajili ya kutuwezesha kupata kitu fulani kwa faida ya watu wetu na sheria ongozi ni zile ambazo tunazitunga kwa ajili ya kutuongoza kutimiza jambo fulani, lakini kwenye kutimiza majambo hayo inawezekana tukakumbana na mambo mengi sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, leo nataka nichangie jambo moja tu kwa sababu sasa hivi Bunge zima pande zote tunakubaliana, kila mtu anakubali kwamba kuna umuhimu mkubwa sana wa mradi mkubwa huu aliouanzisha Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli wa Stiegler’s kwenda kuutekeleza ili kutatua changamoto za umeme zilizoko nchini kwetu. Tuko kwenye Wizara ya Utalii, tunaambiwa, tuliambiwa miaka mitatu nyuma nchi hii Tanzania kwa vivutio duniani ni ya pili, lakini leo hii sio ya pili ni ya nane. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hizi sio taarifa zangu, ni ya nane, sababu kubwa ni sababu miongoni mwa huduma zetu ni mbovu, miundombinu ni mibovu, umeme sio wa uhakika, ndege hakuna, mambo mengi ambayo yapo tumeshuka mpaka wa nane kwa kuwa na vivutio vya utalii. Kwa hiyo, niseme tu nitazungumza hapa kwa sababu, kuna upotoshaji mkubwa sana kama vile huu ukataji miti ambao unaenda kuiharibu Tanzania nzima. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, wewe mwenyeji wa Dodoma, hata UDOM lilikuwa pori, lakini kwa maslahi ya umma tuliamua tujenge Chuo Kikuu na ndio maana mpaka leo unaona tembo kila ikifika msimu wake wanapita pale zilikuwa njia za tembo. Hata wale wazee wa zamani wanajua Dar es Salaam ilikuwa pori pia, lakini leo Dar es Salaam imejaa maghorofa, tumeharibu mazingira. Alisema ndugu yangu Mheshimiwa Getere hapa, kati ya mazingira na binadamu nini ni muhimu? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mbaya zaidi naumia sababu Wabunge wa Tanzania tunazozitoa ndio sababu zilezile wakoloni wetu walizitumia kutukwamisha kutengeneza miradi hii wakati wa Mwalimu Nyerere. Kama kuna Mtanzania anahisi kama walioendelea, nchi zilizoendelea zinafurahia siku moja nayo Tanzania waione imeendelea anajidanganya. Wanatamani sisi tuendelee kuwa hivi hivi maskini na wao waendelee kuwa matajiri. Ndio maana kwenye miradi yote mikubwa inayotaka kutuhakikishia kwenye kuongeza uzalishaji nchini kwetu na kujikwamua kwenye umaskini hawataki kuisikia. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, leo ingekuwa mradi ule kutekeleza condom ungesikia hela zinamiminika. Ingekuwa suala la vyandarua vya mbu hela zinamiminika, lakini mradi ule tunakwenda kuzalisha umeme zaidi ya megawati 2,100 ni umeme mwingi tutaupata ndani ya miaka mitatu ambayo tuna miaka 57 ya uhuru mpaka leo nchi hii tuna megawati 1,400 tu, leo mtu anakuja kukejeli pale, nashangaa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nashauri somo la uzalendo lianze kuanzishwa haraka sana kuanzia chekechea ili watu waijue nchi yao, waweze kuitetea nchi yao, pale tunapokandamizwa. Hivi kuna uharibifu unaofanywa kama mataifa yaliyoendelea? Iraq ilikuwa vile? Ule uharibifu uliofanyika Iraq, Libya, unafanana na uharibifu ule wa pale?

Mheshimiwa Spika, nashukuru sana. Asante sana.