Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Kabwe Zuberi Ruyagwa Zitto

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Kigoma Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. KABWE Z. R. ZITTO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Spika, katika ukurasa wa 21 wa Hotuba ya Waziri amezungumzia inaanzia ukurasa wa 20 kuhusu usimamizi wa Pori Tengefu la Kilombero na amesema kwamba kuna miradi kadhaa inaendelea katika pori hili ikiwemo Mradi wa Umeme wa Maji Rufiji (Rufiji Hydro Power Project) na ninanukuu Waziri anasema; “Pamoja na umuhimu huo bonde hilo linakabiliwa na changamoto za uvamizi kwa ajili ya shughuli za kibinadamu.” Moja ya shughuli ya kibinadamu zinazoendelea kule Mhifadhi Spika Job Ndugai ni pamoja na ujenzi wa bwawa la kuzalisha umeme megawati 2,100. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ninapenda niwe very clear, hakuna mtu anayepinga nchi yetu kuongeza uwezo wa kuzalisha umeme. Lakini tunataka taratibu za kisheria, taratibu za utunzaji wa mazingira na kuhakikisha ya kwamba nchi haiathiriki kwa ujumla wake kutokana na mradi mmoja tu ambao tayari una mbadala mbalimbali kama jinsi ambavyo tukiwa tukielezwa hapa toka jana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Nape amezungumzia kwamba Selous inategemea watu takribani mikoa mitano na pamoja na kwamba ukikata miti ambayo inakatwa ambayo ni sawasawa na size ya Mkoa wa Dar es Salaam; Mkoa wa Dar es Salaam una square kilometers 1,360 na miti inayokwenda kukatwa ni square kilometers zaidi ya 1,400 kila Mbunge hapa afumbe macho aitazame Dar es Salaam yote, aione namna ambavyo ikiwa haina kitu kabisa jinsi ambavyo itakavyokuwa na mbaya zaidi eneo ambalo miti hii inakwenda kuondolea ndiyo eneo ambalo lina unyevunyevu ambao nyakati ambazo wanyama wanatafuta maji ndiko ambako wanakwenda. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sitaki kuangalia hiyo angle ya maisha ya watu, nataka kuangalia angle ya uchumi. Kwa mujibu wa mikakati ya nchi tunataka itakapofika mwaka 2025 tuwe na watalii milioni nane kwa mwaka katika nchi yetu wanaoingiza dola za Kimarekani bilioni 16 kwa mwaka. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, watalii hawa hawatakuwa tena Northern Circuit, watalii hawa watakuwa ni Southern na Western Circuit, ukishaenda ukaiondoa Selous yote ukaondoa, maana yake ni kwamba huwezi kufikia hii mikakati. Ni namna gani ambayo tunalinganisha mikakati yetu na mipango ambayo tunaifanya, hasa ukizingatia tuna- alternative, tuna-alternative ya kuzalisha umeme, tuna- alternative ya bomba la gesi ambayo sasa hivi linatumia asilimia sita tu, na juzi hapa dada yangu Mbarouk amesema tusiite, dada yangu Mheshimiwa Subira alisema gharama ya kuzalisha umeme kwa maji ninafuu kuliko kwa gesi. Lakini ni lazima Serikali ikumbuke capital injection the investment unayokwenda kuifanya kwenye huo uzalishaji wa umeme kwa maji ni kubwa mno itakuchukua miaka 30 ku-recover mpaka urudi kuzalisha kwa senti mbili kwa dola kama jinsi ambavyo Serikali inasema. Kulikuwa kuna haja kubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba ni kuombe, jambo hili la TFS kwenda kuangusha miti ile na kuuza yale magogo jambo hili lisamame kwa muda mpaka hiyo masuala ya Environmental Impact Assessment yatakapokuwa yamekamilika tuweze kuona mitigation measures ni zipi. Vinginevyo Serikali iangalie alternative ya uzalishaji wa umeme as upstream na kwenye power master plan ambayo tunayo inaonesha kuna orodha, Mheshimiwa Nassari ameitaja jana ya miradi mbalimbali ambayo imeorodheshwa ambayo itazalisha umeme sawasawa na huo ya Stiegler’s bila kuiathiri Stiegler’s. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nilikuwa naomba jambo hili tuweze kulitazama kwa namna hiyo tunakwenda kupoteza maana kabisa ya kukuza utalii katika nchi. Kama tusipokuwa makini na namna ambavyo tunashughulika na suala la Stiegler’s Gorge.

Mheshimiwa Spika wewe ulivyokuwa mwanafunzi, ulivyokuwa unafanyakazi wanyamapori, umekaa Selous, ulikuwa game warden Selous hebu itazame namna ambavyo tutaondoa hii miti na Selous itakavyokuwa imekufa na historia yako itakuwa imekufa kabisa, kwa hiyo lazima tulitazame jambo hili kwa mapana yake. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lingine ni hili ambalo limezungumzwa na Kamati suala zima la vitalu. Nilikuwa namuomba Mheshimiwa tu ndugu yangu Kigwangalla kwa kuwa tumeona kwamba kuna tatizo la kisheria ambalo limetokea na kwamba maagizo ambayo ameyatoa kwa nia njema kabisa, lakini ni maagizo ambayo yametolewa kinyume na Sheria turejee kwenye status quo na nilikuwa nakuomba uagize Serikali turejee status quo wakati marekebisho mengine yanafanyika ili tusafiri sekta hii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ahsante sana