Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Yussuf Salim Hussein

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Chambani

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. YUSSUF SALIM HUSSEIN: Mheshimiwa Mwenyekiti, Bismillah Rahman Rahim. Kwanza ni-declare interest ni Mjumbe wa Kamati kwa hiyo naunga mkono hoja za Kamati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, sina kawaida ya kupongeza lakini leo nitampongeza Mheshimiwa Waziri na Naibu wake na watendaji wake kwa namna ambavyo Mheshimiwa Waziri na timu yake anakuja sasa kuielewa hii Wizara na kufanya kazi inavyotakiwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia ni-declare interest kwamba ni mtaalam wa misitu, nimesoma na nimefanya kazi, pia ni mtaalam wa mambo ya hoteli, nimesoma na nimefanya kazi. Kwa hiyo, nitachangia kitaalamu zaidi kuliko kisiasa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Tanzania inapoteza hekta 370,000 za misitu kila mwaka kutokana na matumizi mbalimbali. Ukilinganisha na hekta 10,000 zinazopandwa kwa mwaka hujatoa hapo loss percentage, miti inayokufa na itachukua muda gani, utaona ni kwa kiasi gani Tanzania baada ya miaka mingapi tutakuwa hatuna misitu katika nchi yetu na tutapoteza maliasili hii. Maliasili hii ikipotea ndiyo kusema wanyama na wanadamu wa Tanzania watatoweka kwa sababu kutakua hakuna malisho, maji na hakuna kitu chochote. Kwa hiyo, jukumu la upandaji miti na utunzaji wa misitu ni la kila Mtanzania na siyo la Wizara peke yake. Kwa hiyo, Wabunge, taasisi na kadhalika ni lazima tuhakikishe kwamba tunapanda miti ya kutosha na tunaitunza na tunaitumia vizuri kwa faida yetu na faida ya kizazi kijacho. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kufanikisha hili, nimwombe Mheshimiwa Waziri sasa, kwa upande wake haya ni majukumu yake, tuna vijiji zaidi ya 13,000 Tanzania na vijiji na Serikali za Mitaa huko ndiyo zinamiliki 52% ya misitu, nani anaitunza, anashauri na anawaelekeza matumizi endelevu ya misitu? Tunapaswa kuwasomesha watu na kuhakikisha kwamba kila kijiji na halmashauri ina mtaalamu wa misitu ili atoe elimu inayofaa ya matumizi mazuri ya misitu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Watanzania idadi yetu inaongezeka na mahitaji yanaongezeka kila siku. Kwa hiyo, ni lazima tuhakikishe kwamba miti hii tunaitunza vizuri kwa faida yetu. Mtu akikwambia hajui faida ya msitu huyo anajidanganya maana yake mlango katika nyumba yake ni misitu, lakini nije mwisho tu siku anapoondoka duniani awe Muislamu, awe Mkristu ataondoka na ubao tu. Kwa hiyo, ni lazima suala hili tuliangalie vizuri sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna mabibi na mabwana misitu 672, imeelezwa katika ukurasa wa 45 wa kitabu hiki. Mheshimiwa Waziri ni dhahiri kwamba bado tuna kazi kubwa ya kufanya. Tuboreshe Chuo cha Misitu Olmotonyi, Chuo cha Nyuki Tabora na Chuo cha Mbao pale FITI Moshi ili kupata wataalam wengi wa masuala haya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nije katika sekta ya utalii ambayo ni sekta ngumu sana. Ni sekta tete sana na ndiyo maana nimekupongeza kwa sababu umetulia na ukataka kujua sasa katika sekta hii kuna nini. Tanzania tumeelekeza nguvu zetu katika utalii kwenye mbuga tu. Katika kitabu hiki amegusagusa tu utalii wa fukwe, lakini tujiulize siku ikitokea interaction ndogo tu katika mbuga watalii wakakaa mwezi mmoja au miwili hawataki kwenda huko kwa sababu yoyote tu, tunategemea wapi wakati asilimia kubwa ya pato la Taifa tunategemea kwenye utalii?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri na Serikali naomba mkae na mpange namna gani mtawekeza katika ukanda wa bahari kuanzia Mtwara mpaka Tanga kuona tunaweka hoteli na tunaboresha vituo vya kitalii pale. Kuna utalii wa fishing, kuna diving, kuna snorkeling, lakini kuna utalii ule wa fukwe ambao ni mkubwa sana, hatujawekeza huko tunaelekea upande mmoja. Biashara ya utalii ni biashara ambayo inaweza ikayumba wakati wowote kwa sababu ndogo sana. Kwa hiyo, ni lazima tuwekeze sehemu zote kwa usawa kabisa vinginevyo tutakuja kujikuta tumetumbukia katika dimbwi ambalo siyo zuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini biashara hii inahitaji wataalam. Kwa hiyo, nasisitiza tena Chuo kile cha Utalii lazima kitoe wataalam wa kutosha ambao wataweza kuwahudumia wageni wetu. Mtalii anapokuja hapa haangalii amelala katika hoteli ya ukubwa gani, anaangalia ile service anayopewa hata kama amelala katika chumba kimeezekwa makuti lakini anaangalia ile service. Bila ya kuwa na wataalam waliofundishwa, ni dhahiri kwamba wageni wetu watakapokuja hapa watakosa zile huduma zinazotakiwa na wakizikosa itakuwa hatupati ile tija tuliyoitaka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunategemea tufike watalii 2,000,000 au 3,000,000 ikifika 2020-2030, linawezekana hilo kama tutahamasisha utalii wa baharini. Ukanda wa bahari tukihamasisha basi tunaweza kufikia hapo katika kipindi kifupi sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuwekeza huko katika ukanda, katika kuhamasisha ndiyo Mheshimiwa Waziri na Naibu wako, Katibu Mkuu, mtoke sasa muende nje, lazima tupate serious investors. Tukipata serious investors wakawekeza katika ukanda huo na wakahamasisha hilo maana yake wale wageni watakaowaleta ni wa daraja la kwanza na daraja la pili. Hivyo, idadi ya fedha tutakayopata itakuwa ni kubwa zaidi kulingana na wageni labda milioni tano, sita ambao watakuja, hawa wageni vishuka wanaokula mihogo ya kuchoma barabarani. Kwa hiyo, tuwe na serious investors ili walete wageni ambao wataleta fedha nyingi katika nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu kengele umeshanipigia nimalizie kwa kumshauri Mheshimiwa Rais kajenga Uwanja wa Ndege Chato, ni vizuri sana na navyoamini utatanua utalii katika ukanda ule na hiyo ndiyo nia lakini kujenga uwanja wa ndege tu kama hataboresha zile barabara…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)