Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Muhammed Amour Muhammed

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Bumbwini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. MUHAMMED AMOUR MUHAMMED: Mheshimiwa Spika, nianze kwa kukushukuru wewe binafsi kwa kunipatia nafasi ya kuchangia mada iliyopo hewani. Naomba kuchangia namna wavuvi wanavyotozwa na kudhalilishwa na Wizara ya Uvuvi nchini.

Kwanza kuchomwa kwa nyavu zao. Kumekuwa na utaratibu mbaya sana wanaofanyiwa wavuvi wetu, wanaokamatwa na nyavu za aina fulani kwa kuchomewa moto, dau lake ni moto na kila kitu moto. Hivi kweli ni haki wananchi kufanyiwa hayo katika nchi yao? Kwani hapa Tanzania hakuna Mahakama?

Mheshimiwa Spika, lingine ni leseni ya wavuvi. Kumekuwa na manyanyaso makubwa hapa kwamba ni watu wa aina ipi katika chombo cha uvuvi wanaopaswa kuwa na leseni. Ni chombo, nahodha, mabaharia au vipi? Matatizo haya huletwa hasa na JWTZ na kusababisha madhara makubwa, vipigo na mara nyingine JWTZ huwanyang’anya wavuvi samaki wao baharani eti kwa kuwa hawana leseni ilivyo sahihi. Wakati mwingine wavuvi kutoka Zanzibar hulazimishwa kukata leseni ya kutoka Zanzibar na wakifika Bara haitakiwi wakati mwingine. Usahihi ni upi?

Mheshimiwa Spika, katika mitungi ya gesi hapa napo pana matatizo. Kwa kipindi kirefu wavuvi wamekuwa wakinyang’anywa mitungi yao. Kimsingi hakuna sababu.

Wao wamenunua mitungi kwa ajili ya kuvulia na leo wananyang’anywa. Kama wametenda kosa, sheria ichukue nafasi yake, siyo kuwaonea.

Mheshimiwa Spika, lingine ni mifugo, hivi ni kweli vifaranga vile vilivyotiwa moto ilikuwa ni sahihi? Naomba Mheshimiwa Waziri atapokuja kutoa maelezo, anipatie majibu.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.