Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Dr. Immaculate Sware Semesi

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. DKT. IMMACULATE S. SEMESI: Mheshimiwa Spika, katika ukurasa wa 100 wa hotuba ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi kipengele (c) kimeongelea juu ya ukaguzi wa ufanisi wa kazi katika Kitengo cha Hifadhi za Bahari na Maeneo Tengefu (MPRU). Mheshimiwa Waziri anaelezea hatua za kuvunja Bodi ya Wadhamini na kumsimamisha kazi Meneja wa Kitengo cha Hifadhi ya Bahari na Maeneo Tengefu kwa vigezo vya matokeo ya ukaguzi wa Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (Performance Audit/CAG).

Je, imekuwaje Waziri akimbilie kufanya maamuzi kama haya? Mbona Mawaziri wengine katika sekta zao hawakufanya maamuzi haya? Performance Audit zimefanyika kwa taasisi mbalimbali za Serikali na malengo yake yalikuwa ni kuboresha. Je, Mheshimiwa Waziri aliwapa nafasi ya kujibu yaliyojitokeza? Ripoti ya CAG haioneshi maeneo ya ukaguzi wala vigezo vilivyotumika katika kufanya hiyo performance audit. Pia ripoti hiyo haielezi chochote kuhusiana na udhaifu uliotajwa.

Mheshimiwa Spika, katika miaka miwili mfululizo MPRU haikutengewa kiasi chochote cha fedha kutoka Serikalini. Iweje Wizara itegemee MPRU kufanya utofauti chanya?

Mheshimiwa Spika, katika ukurasa wa 113 na 114 wa kitabu cha hotuba imeonesha utekelezaji wa majukumu ya hifadhi za bahari na maeneo tengefu chini ya MPRU. Hotuba imebainisha utekelezaji wa kazi zake (MPRU) pamoja na malengo yake ya kuendeleza mipango kazi yake kwa mwaka 2018/2019; je, ni kwa nini Wizara haikubainisha kushindikana kwa MPRU kutekeleza majukumu yake kwa ulinganifu wake na matokeo ya ukaguzi wa CAG?

Mheshimiwa Spika, natambua kuwa MPRU hukusanya maduhuli ya takribani slingi bilioni moja kwa mwaka na kwa mwaka wa fedha 2017/2018 mwezi Machi, 2018 yalifikia shilingi bilioni 1.1. Je, uamuzi huu wa Mheshimiwa Waziri wa kuvunja bodi na kumwondoa Mkurugenzi kunatuhakikishiaje maboresho ya mapato?

Je, maamuzi yaliyofanywa na Mheshimiwa Waziri ni sehemu ya mapendekezo ya CAG? Kama siyo, yanasaidiaje katika utekelezaji wa mapendekezo ya CAG na maslahi mapana ya Kitengo?