Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Desderius John Mipata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. DESDERIUS J. MIPATA: Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja na nina mchango ufuatao:-

Mheshimiwa Spika, Wizara hii ni muhimu sana kwa maendeleo ya kiuchumi na kijamii na ina mchango mkubwa kwa maendeleo ya nchi. Hata hivyo, fursa nyingi hazitumiki vizuri na wananchi wa ngazi ya chini yaani wananchi wa kawaida wanashambuliwa badala ya kuelemishwa. Maafisa waliopewa dhamana ya kulinda na kusimamia sheria wameondoka kuwa binadamu na sasa wanapomkuta binadamu anatumia rasilimali hii, kwa namna ya makosa haelimishwi badala yake ananyanyaswa.

Mheshimiwa Spika, nashauri elimu ikitolewa vizuri binadamu atakuwa mlinzi mzuri wa rasilimali za majini. Tabia ya kuwashambulia, kuwaka na kuwatesa sababu ya samaki wawili/watatu si sawa. Walitoka wapi hawa, wanaagizwa na nani?

Mheshimiwa Spika, kuhusu ufugaji wa samaki haujajionesha kama ni kipaumbele, naomba Wizara ijitahidi kutoa elimu.

Mheshimiwa Spika, Ranchi za Taifa, Nkasi tunayo Kalambo Ranch, haina mtaji wa kutosha na mifugo iliyopo ni michache sana. Ranchi ni kubwa lakini mifugo ni michache na hakuna mtaji na miundombinu mingine ya kuimarisha ufugaji. Ranchi haina gari, watumishi wachache na vilevile haitengewi bajeti ya maendeleo na Serikali ili kuboresha ufugaji.

Mheshimiwa Spika, kuhusu mikopo kwa wavuvi, katika Jimbo la Nkasi Kusini wavuvi hawajapata mikopo ya kuboresha uvuvi na hivyo uvuvi unaoendeshwa ni wa kizamani sana na hauna tija.

Mheshimiwa Spika, ufugaji wa samaki, naishauri Wizara kutenga bajeti kuwasaidia wananchi wa Kata za Ninde, Kizumbi, Wampembe na Kala walioko kandokando ya Ziwa Tanganyika, waelimishwe namna ufugaji wa samaki ili kunusuru maisha yao kwani operation zinazoendelea wananchi hawa wanatii sheria na katazo la Serikali.