Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Spika, suala la uvuvi haramu, jambo hili ni vyema likatolewa tafsiri sahihi vifaa ndio haramu au watu ambao ndio wavuvi ndio haramu kulingana na mkanganyiko uliopo katika maeneo mengi nchini na suala la kukomesha lifuate taratibu, sheria na haki za binadamu.

Mheshimiwa Spika, suala la kuchomea wavuvi nyavu; utaratibu wa kutokomeza uvuvi haramu muafaka wake sio kuchoma nyavu kwani kwa kuchoma nyavu ni kusababisha wavuvi kupata umaskini pia jambo hili linatakiwa kudhibitiwa viwandani na sio ziwani au bandarini.

Mheshimiwa Spika, kuhusu tozo za kero kwa wavuvi, ni vyema Serikali ikapitia tozo zote ambazo ni kero kwa wavuvi wetu kwani suala la uvuvi nalo linachangia pato la Taifa letu na pia kupata kitoweo kwa wananchi wetu wa Tanzania.

Mheshimiwa Spika, suala la utaratibu mbovu wa kusafirisha mifugo, kulingana na changamoto wanazokutana nazo wafugaji, mfugaji anapokuwa anatoa na kupeleka mifugo yake mnadani hata kama ni wachache wanamtaka kusafirishwa kwa gari (lori sio sawa).

Mheshimiwa Spika, leseni ya wavuvi itolewe moja kwa moja kwa kila ziwa au bahari. Jambo hili limekuwa na changamoto kwa wavuvi kwani kwa sasa leseni zinatolewa kwa kila Halmashauri jambo ambalo ni gumu kwani samaki wanahama kutoka Halmashauri moja kwenda nyingine.

Mheshimiwa Spika, suala la operation zinazoendelea zinaleta madhara makubwa sana kwani haifuati haki za binadamu, haki za wanyama pamoja na kupeleka migogoro.

Mheshimiwa Spika, mifugo mingi inayokamatwa haipewi matunzo mazuri kama vile chakula na maeneo ya kutunzia inakuwa sio rafiki na kusababisha mifugo hiyo kufa na kusababisha maumivu kwa mfugaji.

Mheshimiwa Spika, kutopelekwa kwa pesa ya maendeleo, hakuna shughuli yoyote inaweza kufanyika bila kupeleka fedha iliyotengwa kwenye eneo husika ili kazi ilivyokuwa imetengwa ikienda kwa wakati ni rahisi kumaliza changamoto zilizopo.

Mheshimiwa Spika, nashauri kutenga maeneo ya wakulima na wafugaji ili kuondokana na migogoro iliyopo katika nchi yetu.