Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Selemani Said Bungara

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Kilwa Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. SELEMANI S. BUNGARA: Mheshimiwa Spika, kwanza namshukuru Mwenyezi Mungu Subhanah Wataalah. Pili, naishukuru Serikali ya CCM kwa kutufikisha hapa tulipofikishwa.

Mheshimiwa Spika, juzi niliwaambia Waheshimiwa Wabunge kwamba hata firauni alikuwa mbaya, lakini watu wake waliokuwa nyuma yake, wanamuunga mkono. Sasa huyu firauni aliota ndoto kwamba ataondolewa katika ufalme wake na akaamua kwamba kila nyumba kumi kuwepo na watu, kila atakapozaliwa mtoto wa kiume auliwe ili ufalme wake uendelee. Bahati nzuri akazaliwa Musa akamlea yeye mwenyewe na ndio yeye akamwangamiza. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hii ina maana kubwa sana Waheshimiwa, hayo mnayoyatetea katika upande wa Serikali ya CCM, leo Waheshimiwa wawili wamesema CCM tunakufa eeh! Na mimi naamini kwamba CCM itajiua yenyewe kama alivyosema Nyerere. Naomba sana Serikali ya CCM muendele na hayo mnayoyafanya. (Makofi/Kicheko)


Mheshimiwa Spika, pia Serikali ya CCM mnatutaka Wapinzani lakini hamtutaki, lakini sisi hatuwataki lakini tunawapendeni. Tukiwaambieni maneno mazuri ndiyo tunawapenda hivyo, mfanye. Mkifanya tu mambo mazuri tu Tanzania, naomba sana Serikali ya CCM muwe wasikivu, moja hiyo.

Mheshimiwa Spika, nizungumzie habari ya mifugo kwanza, Kilwa mmetuletea mifugo, tulikuwa hatuijui mifugo tunashukuru sana sasa hivi tunapata maziwa mengi, lakini hamjawatendea haki wafugaji walikwenda kule, hawana malambo wala hakuna majosho. Naomba sana Serikali ya CCM kwa kuwa mliwatoa mlikowatoa kuwaleta Kilwa hebu tuleeteeni malambo na majosho ili wakae vizuri wale wafugaji, hilo ni ombi la kwanza hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ombi la pili kwetu Kilwa tuna maeneo ya ng’ombe wale, kuna vijiji vingine vimeambiwa wafuge ng’ombe wengine wawe wakulima Mheshimiwa Ulega najua. Kwa mfano, kijiji cha Nakiu ni kijiji cha wakulima lakini kuna ng’ombe siyo chini ya 2000 tunawaomba kila siku ng’ombe hao waende katika sehemu husika hawaendi, tatizo kubwa inawezekana viongozi wa Mkoa na Wilaya kama wamepata rushwa hivi, Mkuu wa Mkoa huyu na Mkuu wa Wilaya ninawasiwasi wamepata rushwa, kwa sababu Mkuu wa Wilaya kaandika barua kwamba ng’ombe wa kijiji cha Nakiu watolewe mwezi wa Novemba waondoke, lakini mpaka leo hawajatolewa na ukimuuliza Mkuu wa Wilaya anasema hela za kuwatoa sina. Ukiwaambia polisi wakawatoe wanasema hela hatuna na kijiji cha Nakiu kimewahi kutoa shilingi 1,500,000 kuwapa polisi kwamba hawana posho, hela wamechukua ng’ombe wapo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Serikali hii sasa Jeshi la Polisi hawana uwezo mpaka kijiji kitoe hela kiwape polisi, hela wamechukua na ng’ombe mpaka leo wapo, kweli hii Serikali, kwamba polisi hawana hela mpaka wanakijiji watoe hela na wanatoa hela halafu ng’ombe hawajatolewa? Mkuu wa Wilaya kala rushwa, Mkuu wa Mkoa kala rushwa, polisi wamekula rushwa na kama hawakula rushwa tuwaone ng’ombe watoke, leo bila hivyo wamekula rushwa! (Makofi/ Kicheko)

T A A R I F A . . .

MHE. SELEMANI S. BUNGARA: Mheshimiwa Spika, kwanza napenda kusema na nipe dakika moja tu nisema. Nimesema kijiji kimetoa fedha kwa ajili ya kuwapa polisi kuja kutoa ng’ombe, lakini fedha wametoa na ng’ombe hawakutolewa kwa mazingira haya nina wasiwasi watu wamepewa rushwa na kama kutoa rushwa basi ng’ombe wale watoke, kama hawakutoka wamepewa rushwa. Ndiyo hoja yangu mimi, nina uhakika kijiji kimetoa hela na ng’ombe hawajatoka. Sasa kama hawajatoka hela ile ndiyo rushwa, sasa kama wewe unasema habari hizi ni za uongo thibitisha wewe, tuende kijijini mimi na wewe kama hela hazikutolewa.

Mheshimiwa Spika, mimi mwanasiasa eeh!