Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa fursa na nianze kwa maneno yafuatayo:-

Mheshimiwa Spika, kabla sijaingia Bungeni kwanza nilipewa kadi ya Chama cha Mapinduzi mwaka 1995, kwa hiyo, mimi ni CCM kwanza kabla ya Ubunge. I am putting this on record. Katiba ya Chama changu sehemu ya kwanza kwenye madhumuni ya kuanzishwa Chama cha Mapinduzi, dhumuni namba saba linasema: “Kusimamia haki na maendeleo ya wakulima, wafanyakazi na wananchi wengine wenye shughuli halali za kujitegemea na hasa kuona kwamba kila mtu ana haki ya kupata malipo yanayostahili kutokana na kazi yake.” (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimesoma dhumuni hili kwa makusudi kabisa ili Serikalini wajiulize swali, je, wanatimiza wajibu wa wanachama wa CCM zaidi ya milioni sita/saba/ nane ambao walikaa kwenye foleni na kuomba kura za nchi hii ili kuweka Serikali madarakani? (Makofi)

Ninarudia, mahusiano yaliyopo kati ya Serikali na wananchi ni mahusiano kati ya principal and agent. Mkataba uliopo kati ya Watanzania na sisi, ni CCM na wananchi na siyo Serikali na wananchi. Chama kimepigiwa kura, tumemnadi Mheshimiwa Rais Magufuli tukampa dhamana ya kuunda Serikali, akasimamie na Serikali yake maslahi ya wananchi wa nchi hii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba niulize maswali yafuatayo; juzi tumepitisha bajeti na kwa masikitiko makubwa sana tutapisha na hii, ndiyo kawaida yetu. Jana tumepitisha bajeti ya kilimo; kilimo kinachangia asilimia 30 ya GDP ya nchi hii, kilitengewa 0.8% ya bajeti ya maendeleo. mifugo na uvuvi inachangia 7% tumewatengea 0.04% ya bajeti ya maendeleo. Halafu tunakuja hapa tunasema kuna kuharibu mazingira, this is nonsense. Hamna lugha nyingine ya kutumia zaidi ya hii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba unisikilize kabisa, leo hii tumezuia wavuvi wasivue, haturuhusu wavuvi wavue kwa kutumia makokoro, sawa, what is the option? Tumetenga shilingi ngapi ya kwenda kuwafundisha wavuvi wetu ili waanze uvuvi wa kufuga wenyewe walioko kando kando ya Ziwa Victoria? Tumewaandaje? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nataka nikwambie jambo la kusikitisha, mkulima mahindi yake leo shilingi 150 kwa kilo. Na mimi nakushuru sana, umetoa maelekezo kwamba Wizara ya Kilimo na Wizara ya Fedha ije kwenye Kamati ya Bajeti. Tumeanza nao vikao, na mimi nakuahidi, tusipoelewana tutarudi humu ndani. Hatuwezi kuendelea na business as usual. Haiwezekani Serikali inashindwa kutimiza wajibu wake, tunaenda kuwaadhibu wananchi. We cannot allow this! Sekta ya mifugo bajeti ya mwaka 2017 development budget tumepeleka asilimia ngapi? Zero! Sifuri. Bajeti ya kilimo tumepeleka asilimia ngapi? Asilimia 18.

T A A R I F A . . .

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Spika, namheshimu na nimefunga. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nataka kushauri mambo yafuatayo: Kwanza, nikizungumzia Sekta ya Mifugo. Ninaongea kuhusu Sekta ya Mifugo kwa mambo makubwa mawili. Moja, nimezaliwa ndani ya mifugo ndiyo sababu naifahamu. Toka mwaka 1983 hakuna proper breeding programme iliyofanywa na Serikali ya nchi yetu. Hakuna!

Mheshimiwa Spika, Serikali ya Mwalimu Nyerere iliandaa sehemu zinazoitwa holding ground kwa ajili ya breeding programme. Kwangu Nzega na Jimbo la Selemani Zedi, kulikuwa na eneo linaitwa Kisasiga. Kule kwetu tuna ng’ombe zinazoitwa Tarime, Waziri anazijua. Ni ng’ombe ndogo, ngozi yake ni nyembamba, lakini zinaweza ku-survive kwenye ukame. Mwalimu akasema ili nimwongezee value huyu Msukuma, akaleta ng’ombe aina ya borani, akaziweka Kisasiga. Mwaka 1990 ziliuzwa kubinafisisha zote hadi ardhi. Pale pamebaki open, hakuna chochote. Mkoa wa Tabora kuanzia Nzega kwenda Tabora Kaskazini kwenda Urambo, kwenda Sikonge, kwenda Wilaya zote zaidi ya asilimia 60 ni hifadhi. Hawa wafugaji wanaenda wapi? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, unajua jambo linalonisikitisha, nami nataka nirudie humu ndani, Serikalini hatuna nia mbaya na Mawaziri, hapa kuna politics ya ajabu sana, mimi sio mwenyeji ndani ya Bunge, nina miaka miwili tu. Mbunge akisimama akiongea, atakuwa branded a name aidha, anamchukia Mheshimiwa Dkt. Magufuli. Simchukii Mheshimiwa Dkt. Magufuli, I have voted for him, I have campaigned for him for sixty days. Na mimi kama Rais Magufuli asingekuwa mgombea wangu mwaka 2020, I didn’t care. Nisinge-care kusema haya ninayosema ndani ya Bunge kila wakati, but because I know he is my candidate, nitasema as far as nimo ndani ya Bunge hili. Nataka niwaombe hii bajeti turudishe. Bajeti hii irudi na siyo kwa nia mbaya. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, leo wafugaji wanauawa, nataka nikupe kichekesho. Kule Nzega wanakata leseni ya kufanya biashara. Namshukuru Mheshimiwa Waziri, ukimsumbua anakusaidia. Anakata leseni ya kusafirisha ng’ombe, inaitwa kabisa leseni ya kusafirisha ng’ombe nje Mkoa wako, analipa na mapato na kila kitu, akifika hapo Nala anakamatwa. Anakamatwa mama aliyebeba kuku 200 anazipeleka Dar es Salaam, anaambiwa alipe faini ya two million. What is this? Nchi yetu leo mkulima ananyanyasika, mfugaji ananyanyasika, mvuvi ananyanyasika, machinga ananyanyasika na mfanyabiashara ananyanyasika. This is unfair and we should not allow it.

Mheshimiwa Spika, nakushauri unda Tume ya Bunge, mimi sio mtalaam wa Kanuni. Jambo la kusikitisha, nataka nikwambie jambo, Mheshimiwa Nape aliandaa Hoja Binafsi inayohusu wafugaji. Hizi Kanuni za ajabu tuzibadilishe kwa maslahi ya nchi yetu na chama chetu. Tukaitwa kwenye Kamati yetu ya Uongozi ya chama chetu. Nataka nikwambie, hata kama tukifuata kanuni na taratibu zote, hoja zinazohusu wananchi zinaenda kufia kwenye Kamati za Vyama. Why are we here? (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Spika, nataka niseme, kama tumeamua kuwa na mfumo wa demokrasia ya vyama vingi ambapo vyama hivi vinatuleta ndani ya Bunge, tuna mihimili mitatu, kila mhimili utimize wajibu wake kwa maslahi ya Taifa hili.

Mheshimiwa Spika, nataka nimwambie ndugu yangu Mpina, hapa mkononi nina document nitamkabidhi. Leather sector tunaye mwekezaji amekuja ana kiwanda kikubwa sana Ethiopia. Tunasema industrialization, kama hatu-invest kwenye sekta ya kilimo na mifugo, let us forget about industrialization. Wizara ya Fedha inazungumzia 3.9% ya inflation. Mnajua bei ya bati ni shilingi ngapi? Ni shilingi 30,000, ng’ombe shilingi 150,000, mahindi shilingi 150, halafu tunasema tuna-control inflation kwa kuwatia umaskini watu.
We should not allow this. Sekta ya leather…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)

Mheshimiwa Spika, nakushukuru.