Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niwapongeze Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri na naunga mkono hoja.

Mheshimiwa Naibu Spika, nina hoja moja tu. Wilaya ya Mpwapwa ina taasisi mbili za mifugo. Taasisi ya Utafiti wa Mifugo na Chuo cha Mifugo. Taasisi ya Utafiti wa Mifugo ndiyo Makao Makuu ya nchi nzima katika utafiti wa mifugo. Taasisi hii ina ng’ombe zaidi ya 800, lakini hawana vitendea kazi. Wana mashamba ya kulima majani kwa ajili ya mifugo, wana trekta moja na limechakaa na wana Lorry moja, nalo limechakaa. Sasa ili ng’ombe wapate chakula, watalima yale mashamba kwa majembe ya mkono? Kwa hiyo, naomba ile taasisi ipewe fedha za kutosha. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Chuo cha Mifugo, mwaka 1995 yale mabweni tulitaka tuyachukue sisi Halmashauri tuyakarabati iwe Shule ya Sekondari lakini Wizar ikayawahi. Sasa yamechakaa tena. Itolewe bajeti ya kutosha mabweni yakarabatiwe na ile Taasisi ya Mifugo ya Mafunzo iongezewe bajeti na ile maabara iongezewe vifaa.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana na naunga mkono kwa asilimia mia moja.