Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Agnes Mathew Marwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. AGNESS M. MARWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kunipa nafasi hii ili nichangie Wizara hii kwa sababu na mimi pia ni mvuvi. Kwanza nianze kwa kumpongeza sana Mheshimiwa wetu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kazi nzuri anayofanya ya kuwatetea Watanzania na kuwajali Watanzania na hasa Watanzania masikini. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia nimpongeze Mheshimiwa Waziri kwa kuchaguliwa katika Wizara hii. Kipekee zaidi nimpongeze Katibu Mkuu wa Wizara hii na Wataalam wake kwa kuwasababishia Watanzania umaskini uliokithiri na hasa Watanzania wafugaji, narudia. Nimpongeze sana Katibu Mkuu wa Wizara hii pamoja na wataalam wake kwa kuwasababishia wavuvi wa Tanzania umaskini uliokithiri. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kabla sijaendelea na mengine nianze kwa kuishauri Serikali. Kutokana na mapato waliyofanya na hasa yale waliyofanya baadhi yao ya unyang’anyi kwa wavuvi hawa niiombe Serikali sasa imuagize CAG aende akakague hizo pesa walizowanyang’anya hawa wavuvi ili iweze kufanya maendeleo mengine.

Mheshimiwa Naibu Spika, pili niishauri pia Serikali kwamba kutokana na kwamba, tuna matatizo mengi sana ya maji, elimu na mambo mengine Wizara hii safari hii kwa bajeti hii isipewe pesa, hiyo pesa iende kwenye elimu na mambo mengine, kwa sababu pesa waliyokusanya, ukisema uwaongezee pesa nyingine ni kwa ajili ya kusafiri na kwenda kuwapiga mabomu ndani ya bahari na ndani ya ziwa wavuvi na wananchi kwa ujumla. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naamini kabisa Mheshimiwa Mpina ananisikia na narudia tena kumwambia Mheshimiwa Mpina ameingizwa chaka na Waziri Mkuu wake.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri ameingizwa chaka na Katibu Mkuu wake pamoja na hawa wasaidizi wake, kwa nini, Katibu Mkuu, yeye ni Mtaalam wa mambo haya na ndiyo maana amechaguliwa kuwa Katibu kwa sababu yeye kasomea. Hata kama Waziri hajasomea mambo haya ya uvuvi basi Katibu Mkuu na wataalam wake wanaelewa; lakini kwa nini wanafanya vitu bila kuangalia shida au matatizo yanayowapata wananchi? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hawa ndio wapiga kura wetu, hawa ndio wapiga kura wa Mheshimiwa Magufuli. Naamini kabisa hata Mheshimiwa Dkt. Magufuli jinsi alivyo active Mheshimiwa Rais wetu akinisikia leo atatuma tume haraka sana iende kuangalia haya mambo, kwa sababu hiki tunachokilalamikia hata Mheshimiwa Rais wakati mwingine haelewi ni nini kinachoendelea huko ziwani. Ni kama wakati ule wa operation ya bomoa bomoa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, wakati wa operation ya bomoa bomoa kuna watu walivyosikia tu bomoa bomoa wakaingia na wengine ambao hata hawakuwa wanafanya au wanabomoa kihalali wakaanza kubomoa hovyo hovyo. Hata hivyo Mheshimiwa Rais kwa sababu ya kuwajali Watanzania, aliposikia vizuri na aliposikiliza kwamba watu hawa wanaonewa alienda kuangalia na kweli sasa watu hawaonewi tena. Kwa hiyo nimwombe sana Mheshimiwa Rais hili suala alichukulie kwa umakini zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niliombe Bunge lako Tukufu liunde kamati kwa ajili ya uchunguzi wa haya masuala ya uvuvi ili kusudi tuwasaidie wavuvi hawa. Wanaumia, wanaumizwa sana, kwa sababu kuna baadhi yao wanachomewa nyumba, wanachomewa nyavu, lakini bila sababu za msingi. Tunakubali kwamba sheria zipo na sheria zenyewe tulizitunga sisi wenyewe, lakini wanapitiliza sasa wanavuka wanaenda nje ya sheria.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo niiombe sana Serikali iliangalie hili suala kwa umuhimu zaidi; kwa sababu kuna mambo mengine yanatokea kwa mfano Mheshimiwa Waziri leo amesema kwamba milipuko imepungua kwa wavuvi haramu. Ni kweli kabisa Mheshimiwa Waziri milipuko imepungua kwa wavuvi haramu, lakini milipuko imeongezeka kwa wale wataalam wake wale wanaokwenda kule kwenye operation.

Mheshimiwa Naibu Spika, wao sasa ndio kabla hawajaenda kuwakamata wavuvi wanaanza kulipua mabomu. Hivi lengo lao ni kwenda kuwakamata au lengo lao ni kuwauwa wananchi? Hali ngumu Mheshimiwa Waziri, wananchi wana maisha magumu, kwa hiyo wananchi wengi sasa hivi wana ugonjwa wa pressure, sukari; hivi wanaposikia yale mabomu wanajisikiaje? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, haya masuala yananiuma sana kwa sababu na mimi nimetokea kwa wavuvi, hawa wavuvi wanapata shida. Wavuvi wa nchi hii, fikiria ukianzia Zanzibar, Dar-es-Salaam, Mara na sehemu nyingine, huu ni uonevu unaopitiliza. Hebu Serikali ichukue hatua za lazima waende wakasaidiwe, waende wakaangaliwe, kwa sababu haya mambo yanayofanywa ni mambo ambayo ni ya uonevu tena uonevu uliokithiri. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kama Mheshimiwa Waziri Mpina, anaona hii Wizara hawezi kuitendea haki Mheshimiwa Mpina amwambie tu Mheshimiwa Rais atoke ili kusudi amchague mvuvi kabisa aende akaangalie haya mambo anaelewa uvuvi. Wakinichagua hata mimi ambaye sijasomea hayo mambo kwa sababu, nilikuwa mvuvi naweza, kuliko hawa wataalam wanadanganya, wanakudanganya.

mimi najua wanamwingiza chaka, Mheshimiwa Mpina ni mtendaji mzuri, lakini wanamwingiza chaka kuna mambo mengine alitakiwa, kwa mfano… (Makofi)

TAARIFA . . .

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa kwa mfano bei za nyavu zile nyavu zinazohitajika kuvuliwa dagaa au samaki zilikuwa kati ya Sh.16,000/= lakini sasa hivi zimefika Sh.45,000/=. Pia kuna maboya ambayo kwa bundle ilikuwa ni Sh.30,000/= lakini sasa ni Sh.130,000/=. Kwa hiyo inaonesha ni jinsi gani haya mambo sasa yanavyokuwa ni magumu kwa hawa wavuvi. Wanachomewa vitu vyao, lakini pia bado wanapewa, wanawekewa tozo nyingi zisizokuwa na sababu au na maana. Pia kuna gharama nyingine ambazo kwa kweli zinakuwa ngumu sana kwa wavuvi na hasa wale wa hali ya chini.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika hili nimwombe sana Mheshimiwa Waziri kama hii leseni kweli aliitoa yeye kwa huyu mfanyabiashara ambaye ni mmoja tu anayetoa na kuuza nyavu hizi; yule Mhindi ambaye yuko Arusha, Mheshimiwa Waziri akaongee naye sasa arekebishe hizi bei kwa sababu hizi bei zinawaumiza hawa wananchi. Kwa hiyo itabidi waendelee angalau kutumia zile, watatumia hata vile vyandarua ambavyo wanapewa wajawazito na watoto wadogo kwa sababu inakuwa ni ngumu sasa kuzinunua ni bei ghali. Kwa hiyo Mheshimiwa Waziri hili suala aliangalie ili kusudi hawa wananchi waweze ku-afford kununua hizi nyavu kwa ajili ya shughuli zao.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri ni mtoto wa mkulima na ni mchapakazi. Mheshimiwa Waziri hili suala la uvuvi na hasa hawa wanaotoza ushuru kwenye magari au wanaotoza ushuru hawa samaki hata yeye mwenyewe anaweza tu akaliangalia hili suala, kwa sababu kwa mfano kuna vibambala. Mheshimiwa Waziri vibambala wale huwa ni samaki wakubwa ambao ni wale Sangara wakubwa kidogo huwa wanataka kuwa kama reject, samaki ambao si fresh sana lakini ni samaki ambao hawaingii kiwandani.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo wale wananchi wanatengeneza vibambala, si samaki wadogo. Sasa Mheshimiwa Waziri kama hata hawa samaki vibambala wanakamatwa na wanatozwa ushuru anategemea nini , kwamba sasa tutakula nini. Au wananchi hawa wafanyabiashara, maana hivyo vibambala wanaouza wengi wao ni wale wamama wajasiriamali wadogo wadogo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo nimwombe sana Mheshimiwa Waziri afuatilie haya masuala kwa ukaribu kama nilivyoshauri, kwamba iundwe kamati maalum toka Bungeni ili iende ikasimamie na kushughulikia haya mambo.

Mheshimiwa Naibu Spika, juzi juzi kuna gari ilikamatwa la kuku. Kuku wana ushuru, hapo Singida. Kuku wamekatiwa ushuru, kutoka tu kituo kimoja kwenda kituo kingine wanataka ushuru mwingine, kutoka kituo kimoja tena kwenda kingine wanataka ushuru mwingine. Mheshimiwa Waziri hivi kweli hata kama ndiyo operation hii ni operation chukua pesa au operation tokomeza? Kwa hiyo, nimwombe sana Mheshimiwa Waziri hili suala aliangalie sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna suala lile la hawa hawa wafanyabiashara wenye mitumbwi. Kwenye mtumbwi anakuwepo boss na wafanyakazi wake. Kwa mfano anakuwepo boss mwenye mitumbwi na wafanyakazi wanaopanda mle kwenye boti wanaokwenda kuvua wanakuwa watano hadi kumi. Sasa kila mmoja anatakiwa awe na leseni, boss awe na leseni, wale 10 ambao pia ni wavuvi wake wanatakiwa kila mmoja awe na leseni.

Mheshimiwa Naibu Spika, hivi Mheshimiwa Waziri katika mazingira haya inakuwaje? Ni kwamba sasa hata kama, mimi siamini kama Mheshimiwa Rais kweli atakubaliana na hili suala kwamba kila mwananchi, hata yule ambaye anaajiriwa aende akakatiwe leseni. Hiyo leseni yeye anaifanyia kazi gani wakati boss wake ana leseni? Au siku hizi labda kuna leseni za vibarua ili uajiriwe lazima uwe na leseni ndipo uajiriwe. Hata kazi za kuvua samaki, hata kazi za kuuza dagaa?

Mheshimiwa Naibu Spika, kama ndivyo basi tunatakiwa hata sisi tuwe na leseni. Mheshimiwa Spika anatakiwa awe na leseni, wewe Naibu unatakiwa uwe na leseni, sisi Wabunge tunatakiwa tuwe tuna leseni ili kusudi ndipo tuingie bungeni.