Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

Hon. Taska Restituta Mbogo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

MHE. TASKA R. MBOGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kumpongeza Mheshimiwa Dkt. Tizeba, Waziri wa Kilimo na Naibu wake Mheshimiwa Dkt. Mary Mwanjelwa kwa kazi nzuri wanayoifanya ya kuendeleza kilimo nchini Tanzania. Niende moja kwa moja kwenye Mkoa wangu wa Katavi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Katavi ni mkoa ambao unazalisha mazao ya chakula na biashara. Sisi Katavi ni miongoni mwa Mikoa ya Nyanda za Juu Kusini inayolisha Tanzania, the big six ambayo ni Katavi, Rukwa, Songwe, Mbeya, Iringa na Ruvuma. Katavi hatuna njaa, tunalima mazao ya kilimo cha biashara na chakula. Mazao hayo ni mahindi, mpunga, alizeti, karanga, pamba, korosho na nyuki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Katavi tumekuwa tukilima zao la biashara la tumbaku kwa muda mrefu sana, ni zao linalotegemewa kwa biashara, lakini zao hilo limekuwa likiwaumiza sana wakulima, afya zao zinaharibika maana tumbaku inashuruba sana kuanzia ulimaji wake, kukausha, mpaka kuuza, kote kuna kazi ya kutumia nguvu. Mkulima anapokuwa amevuna anakuwa ameumia sana. Pia katika uuzaji wa zao la tumbaku kuna shida maana kuna utaratibu wa kupangiwa kilo za tumbaku za kuuza na kila mwaka kilo wanazopangiwa kuuza zinapungua. Hii inawapa shida wakulima, wanapata hasara maana wanachopangiwa kinapungua kila mwaka hivyo basi lipo hitaji la kuongeza zao la biashara Katavi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kilo za tumbaku walizopewa ni kama ifuatavyo:-

(i) Season 2014/2015 walipewa kilo 11,910,459.

(ii) Season 2015/2016 walipewa kilo 8,445,786.

(iii) Season 2016/2017 walipewa kilo 12,099,742. Tumbaku iliyozidi imevunwa ni kilo 2,711,709.

(iv) Season 2017/2018 ambayo inakaribia kununuliwa, makadirio ni kilo 7,452,562.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mahitaji ya Mkoa wa Katavi ni kama ifuatavyo:-

(i) Tunaomba mtuongezee Maafisa Ugani kwa sababu Mkoa wa Katavi asilimia 80 ya mkoa mzima hakuna maafisa hawa. Hivyo, tunaomba tumepewa Maafisa Ugani kila kijiji.

(ii) Maafisa Ugani waliopo ambao ni wachache wapewe mafunzo kuhusu mazao mapya ya pamba na korosho ambayo yameletwa Mkoani Katavi. Kwa sasa hivi Maafisa Ugani waliopo hawana ujuzi wa zao la pamba na korosho.

(iii) Mfumo wa soko wa zao la pamba haujawekwa vizuri maana wakulima wanatakiwa wawauzie vyama vya ushirika. Pia wakulima wa Katavi hawana uelewa wa zao hili la pamba.

(iv) Serikali iruhusu mapema kuuza mahindi nje, sio wasubiri mpaka mahindi yaharibike.

(v) Mkoa wa Katavi tunaomba mbegu za korosho kwa wingi ili wakulima waweze kulima kwa wingi.

(vi) Tunaomba Bodi ya Korosho ituletee mbegu ya korosho Mkoani Katavi.

(vii) Miundombinu ya biashara ni mibovu inafanya wafanyabiashara wanunue mazao kwa wakulima kwa bei ndogo sana.