Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

Hon. Kiza Hussein Mayeye

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

MHE. KIZA H. MAYEYE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa afya njema na kuniwezesha kuchangia leo hii kwa maandishi. Napenda kuanza kuchangia kwa kusema hakuna asiyefahamu kwamba kilimo ni uti wa mgongo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi yoyote duniani ambayo imefanikiwa, kilimo kinapewa kipaumbele kwa asilimia kubwa. Kilimo ndiyo tegemeo la wananchi wengi kwa asilimia 99. Wengi wetu tumefanikiwa hapa leo kwa ajili ya kilimo, wazazi wetu wanategema kilimo, maisha yao yanaongozwa na kilimo lakini leo kilimo hakithaminiwi kabisa kwani changamoto ni nyingi sana, wakulima wanapata shida sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakulima hawanufaiki kabisa na kilimo kutokana na kwamba mkulima analima, anatumia pesa na muda mwingi lakini anapovuna bei zinakuwa ndogo na hazimlipi kabisa ukilinganisha na gharama alizotumia. Leo Mkoa wa Kigoma wakulima wanalima kahawa, kwanza wanatumia gharama na muda mwingi ila anapokuja kuuza anauza kwa bei ndogo. Hii ni changamoto kubwa sana. Serikali iwasaidie sana wakulima kuuza mazao yao kwa bei nzuri lakini pia kuwatafutia masoko ndani na nje ya nchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la mbolea kutofika kwa wakati, mbolea zimekuwa zikichelewa, hazifiki kwa wakati. Wananchi wanateseka sana kwani mbolea zinafika mkulima anavuna. Hivi kweli hapa mnawasaidia wakulima au mnawakomesha? Leo wakulima wa korosho wanalia kwa kukosa sulphur kwa wakati. Niombe sana Serikali suala la mbolea liangaliwe kwa makini, wakulima imefika mahali wanakata tamaa katika mfumo mzima wa kilimo, wanaona bora wasilime lakini kilimo ndiyo tegemeo lao na msaada, wanategemea kusomesha watoto, kupata afya nzuri kupitia kilimo lakini wakulima wamepoteza matumaini kabisa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, viuatilifu vya kuua wadudu. Mazao mengi yanaharibiwa sana na wadudu kama viwavi jeshi, wakulima wanapata hasara kubwa sana. Mtu analima hekta 30 za mahindi lakini anapata hasara ya hekta 10, zinaharibiwa na wadudu. Naomba sana Serikali iwasaidie wakulima dawa za kuuwa wadudu. Watu wanajiua kwa kupoteza pesa, mtu analima hekta 50 anapata hasara kubwa, mazao hayazai, wadudu wanakula. Nchi za jirani zetu Barani Afrika mpaka sasa wametenga pesa kwa ajili ya kukabiliana na wadudu hawa waharibifu kama viwavi jeshi. Niombe sana Serikali itenge pesa sasa za kuhakikisha inawasaidia wakulima katika kupambana na wadudu waharibifu, wakulima wagawiwe dawa za kuulia wadudu na kuzuia. Hii itasaidia sana kupata mazao vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu migogoro ya ardhi na vyanzo vya maji, kumekuwa na migogoro mingi inayotokea katika maeneo mengi. Watu wanauana kwa kugombania ardhi. Niombe sana Serikali isimamie na kuwasaidia ardhi ya kutosha ili kuondoa maafa na migogoro ambayo inazidi siku hadi siku.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Kigoma migogoro ya wakulima kugombania ardhi ni mingi sana katika vijiji vya Kasulu, Pamila, Manyovu na Kibondo. Wananchi wa Kasulu wanazuiwa kulima katika eneo la Kagerankanda wakati wananchi wamelima miaka mingi na ni eneo ambalo wanalitegemea na hata Mheshimiwa Rais alipopita aliwaahidi wananchi kutumia eneo lile lakini wanakuja viongozi wanatoa matamko yao na wanakwenda kinyume na kauli ya Rais. Niombe sana Serikali iwaachie wananchi hawa eneo hili waendelee kulima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, asilimia kubwa ya wananchi wa Kigoma hasa Wilaya ya Kigoma Vijijini wanategemea zao la michikichi lakini zao hili limesahaulika kabisa na linaonekana kama halina thamani. Wenzetu wa Malaysia walikuja kuchukua mbegu kwetu, wamelipa thamani zao hili na sasa ni nchi inayosambaza mafuta duniani. Kwa hiyo, Tanzania tulifanye zao hili kama zao la biashara ukizingatia tunaenda katika nchi ya viwanda, kwa nini tusiwe watengenezaji wakubwa wa mafuta kwani katika michikichi tunapata mafuta mazuri sana kwa afya ya mawese, mise lakini pia kupitia mafuta haya tunapata sabuni nzuri sana za gwanjwi. Naomba Serikali iwapatie wananchi wa Kigoma mbegu bora za michikichi kwani kampuni inayouza miche hii inauza mche mmoja kwa shilingi 5,500, wananchi hawana uwezo wa kununua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sana kuiambia Serikali kilimo ndiyo kila kitu, wananchi wanategemea sana kilimo. Kama kweli tunataka nchi ya viwanda basi lazima Wizara ya Kilimo ipewe kipaumbele, bajeti iwekwe kubwa wananchi wamekata tamaa kabisa na kilimo.