Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

Hon. Amb. Adadi Mohamed Rajabu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muheza

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuchangia hoja hii na naunga mkono hoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kilimo inabidi kipewe kipaumbele sambamba na ujenzi wa viwanda. Wizara inabidi iendelee kubuni mipango ya kisanyansi kama tunataka tutoke katika jembe la mkono, kwa mfano, kilimo cha umwagiliaji, mabwawa na visima viimarishwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, zao la chai ni moja ya mazao ambayo sisi Amani – Muheza linalimwa kwa kiwango kikubwa. Makampuni yanayolima chai Amani ni EUTCO lakini wana tatizo kubwa, wanalima chai hawaruhusiwi ku-pack, ku-brand na kuuza. Wanachokifanya ni kuchakata na kwenda mnadani Mombasa kutafuta soko. Kwa nini twende mnadani nje ya nchi? Kwa nini msiruhusu hawa wenye uwezo ku-pack, ku-brand na kuuza nchini na nje Mombasa, Kenya?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Tanga tunalima katani kwa kiwango kikubwa sana lakini zao hili halijapewa umuhimu wa kipekee ili kuweza kusaidia ulimaji wa zao hili na uuzaji wake ambao kwa sasa soko lake ni zuri kwenye soko la dunia. Aidha, tuna kiwanda cha pamba ambacho kinanunua katani kwa wingi lakini hawana soko kubwa ndani na nje ya nchi. Mipango ifanywe ili kuzuia bidhaa kutoka nje, kukuza soko na kufanya wananchi waweze kulima sana katani. Kampuni hii ya Katani Limited imeingia mikataba na wakulima wadogo wadogo kulima katani na kuwauzia wao kwa bei ndogo. Mikataba hii wananchi wanaumizwa, iangaliwe vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ingeangalia utaratibu wa kutoa mbegu na mbolea bure kwa wananchi. Nimeona mfano kwenye nchi moja jirani ambapo wananchi walivuna mahindi mengi hadi wakaamua kuwauzia WFP/ WHO. Sio lazima Serikali itoe kwa nchi nzima, ingechagua baadhi ya mikoa michache kwa majaribio. Aidha, mikopo ya zana za kilimo itolewe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kulima pamba kwa wingi hapa nchini tatizo kubwa lililoko ni ubora (quality) ya pamba yetu bado iko chini ukilinganisha na nchi zingine ambapo grades za pamba zao ziko juu. Nashauri tuangalie uwezekano wa kuona tutawasaidia namna gani wakulima wetu kuweza kulima pamba yenye ubora.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nasifu sana mradi wa Mkulazi. Mradi huu ingawa sijafanikiwa kuuona lakini ni mradi wa mfano. Tuwe na miradi mingi kama hii itatuvusha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba Wizara ijipange na kuona itasaidia namna gani kuzuia panya wakubwa Mkoani Tanga ambapo walikula mahindi yote. Tafadhali angalieni namna ya kusaidia.