Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

Hon. Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na nia njema ya Serikali kumekuwa na changamoto nyingi sana kwenye sekta ya kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye zao la korosho kuna maswali ambayo bado hayajapata majibu. Kuna mkakati gani wa Serikali wa kuhakikisha uzalishaji wa korosho unaongezeka? Hivi mwisho kabisa wa matumizi ya sulphur ni nini? Kwa nini utafiti ulifanyika taratibu magonjwa mengine ya korosho tukatumia viatilifu vingine ili kuweza kuongeza uzalishaji?

Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa za kampeni za hammers kuhujumu usambazaji wa sulphur liko kila mara, lakini bado hao hao ndio wanapewa tender kila mwaka ya kusambaza viatilifu. Hujuma za msimu uliopita zilitosha kampuni hii isipewe kazi hiyo na wahusika wachukuliwe hatua.

Mheshimiwa Mwwenyekiti, kuhusu suala la malipo ya wakulima, kuna tatizo kubwa sana juu ya malipo ya wakulima juu ya kupokelea pesa zao benki. Bado wananchi hawa wanatakiwa kupewa elimu ya kutosha. Suala lingine ni ucheleweshwaji wa malipo kwa wakulima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tusimamie sana wanunuzi ili wawalipe wakulima mapema, itasaidia kuepukana na hujuma ya kangamba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho kabisa ni kuhusu soko na uuzaji wa ufuta. Kuna mkanganyiko mkubwa sana juu ya biashara hii. Tunataka kushauri kwamba suala la ufuta kuingizwa kwenye stakabadhi ghalani litaleta usumbufu mkubwa sana. Unyaufu sio suala la kufumbia macho kabisa litaleta shida kubwa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ufuta ni zao ambalo lina nyauka kwa haraka sana, suala hili linahitaji utafiti mkubwa sana.