Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

Hon. Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, niipongeze Wizara kwa hotuba iliyoeleza uhalisia na changamoto zinanojitokeza katika kukamilisha utekelezaji wa miradi. Naiomba Serikali ifuate yafuatayo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, iongeze bajeti ya kilimo hasa kwenye miradi ya maendeleo kwa sababu bajeti iliyopo ni ndogo kulinganishwa na ya mwaka 2017/2018. Mazao yote ya kibiashara yapatiwe masoko ndani na nje ili kukidhi mahitaji ya wakulima na kuinua uchumi wa nchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa na uhaba wa pembejeo na mbegu bora, kwa mfano zao la alizeti. Tunaiomba Serikali kuhakikisha inaondoa uhaba huo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna uhaba mkubwa wa maafisa ugani pamoja na vitendea kazi. Tunaiomba Serikali iajiri na kuleta vitendea kazi.