Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

Hon. Willy Qulwi Qambalo

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Karatu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

MHE. QAMBALO W. QULWI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ushirika bado unakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ubadhirifu wa mali za vyama vya ushirika uliofanywa na baadhi ya viongozi na wanachama wasio waaminifu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Ayalabe SACCOS Wilayani Karatu, fedha za ushirika zilifujwa miaka zaidi ya sita iliyopita na hadi sasa hakuna majibu. Waliohusika kupoteza fedha hizo wanafahamika maana fedha zilitoka benki ya TIB na kuingia kwenye account zao. Hapa wezi si wako wazi lakini kwa kuwa wezi wana mtandao ndani ya Wizara bado wameendelea kulindwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wanachama wa SACCOS hii pamoja na viongozi wa Wilaya wamelalamikia sana na SACCOS hii kwamba imeendelea kudorora na wananchi wanakosa imani kabisa na vyama vya ushirika. Leo hii Serikali inajitahidi kufufua ushirika lakini wananchi hawaelewi kutokana na mifano hii mibaya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mrajisi wa Vyama vya Ushirika anatuhumiwa sana na wanachama wa Ayalabe SACCOS kama ndiye anayewalinda wezi hao. Najua jambo hili liko mezani kwa Naibu Waziri wa Wizara hii. Niishauri Wizara ilifanyie kazi tatizo hili ili haki itendeke.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunayo ardhi nzuri na hali ya hewa nzuri kwa zao la alizeti. Hatuna kabisa sababu ya kuagiza mafuta nje wakati tungeweza kulima wenyewe na kuwasaidia wananchi wetu. Serikali iwapatie wananchi mbegu bora ya alizeti.