Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

Hon. Bernadeta Kasabago Mushashu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

MHE. BENARDETHA K. MUSHASHU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Waziri kwa kazi nzuri mnayoifanya kwenye kilimo na ushirika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kilimo ni muhimu sana katika kuleta maendeleo ya Mtanzania. Huwezi kuleta maendeleo ya Tanzania kama wakulima ambao ni asilimia 70 watakuwa wamekosa kuendelezwa/wameachwa nyuma. Kwa sasa kilimo kinacholimwa hakina tija, bado wanatumia zana duni kama jembe la mkono, hawalimi kitalaam, wanalima kilimo cha kujikimu siyo kilimo cha biashara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunahitaji tuwe na Maafisa Ugani ili waweze kuwaelimisha/kushauri wakulima.Kuna upungufu mkubwa sana wa maafisa ugani. Mkoa wa Kagera tuna upungufu wa Maafisa Ugani takribani 500 lakini wako ngazi ya kata. Kata moja ina vijiji vitatu mpaka sita, hana vitendea kazi hana hata pikipiki, atawazungukia vipi wakulima? Napendekeza waajiriwe Maafisa Ugani kwenye ngazi ya kila kijiji. Hawa wakitosheleza wakafanya kazi yao ya ugani, tutainua kilimo, tutapata malighafi ya viwanda katika uchumi wa viwanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, bei ya kahawa ni mbaya sana, kilo moja inauzwa kwa shilingi 1,000. Mbuni ukiupanda utatumia miaka miwili mpaka mitatu kuanza kuzaa kahawa. Zikianza kuzaa unaulea mbuni kwa mwaka mzima ukipalilia, ukiweka mbolea, unapulizia dawa unaishia kupata shilingi 1,000 tu kwa kilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa muda mrefu mkulima wa kahawa ameendelea kuwa maskini kwa sababu ya bei ndogo ya kahawa. Amekata tamaa ya kuendelea kulima kahawa. Serikali imependekeza kuondoa tozo 21 zifutwe. Nawaunga mkono hoja kwa hili lakini ili haya yasibakie kwenye makaratasi tu, baada ya bajeti hii. Wawakilishi wa wananchi (Wabunge) kutoka maeneo yanayolima kahawa tukutane na watalaam, tupitie mpango mkakati wa kupandisha bei ya kahawa kiukweli.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndizi kwa mtu wa Kagera ni zao la chakula, ni zao la biashara ya migomba imeshambuliwa na ugonjwa mbaya wa mnyauko, ni janga. Wakulima wanashauriwa mgomba ukigundulika una mnyauko, anaambiwa kata/ng’oa/zika. Matokeo yake mashamba yamebaki yakiwa wazi/matupu.Migomba imeisha sababu ya kung’olewa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ipo miche ya migomba isiyoshambuliwa na mnyauko. Kwa kiasi kikubwa wanategemea maabara ya Arusha ni mbali sana na Kagera.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kagera kuna Kituo cha Utafiti cha Maruku ambao wanao watalaam lakini hawana maabara kubwa, wanategemea Arusha. Naomba ili kumsaidia mkulima wa Kagera kumuondolea umaskini zitolewe fedha nyingi za kutosha, ili Kituo cha Utafiti cha Maruku waweke maabara kubwa. Wazalishe tissue, culture. Miche safi isiyo na vimelea vya mnyauko isambazwe kwa wakulima wengi waondokane na gonjwa baya la mnyauko.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.